TANESCO Yafanya Jitihada za Kupunguza Makali ya Mgao wa Umeme
Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO Maharage Chande |
Na Mussa Augustine.
Shirika la Ugavi wa Umeme Nchini (TANESCO),limesema wakati
huu wa kipindi kifupi limefanya jitihada
za kupunguza makali ya mgao wa umeme kwa kufanya marekebisho ya mtambo mmoja
ubungo na kusaidia kuingiza megawati 35 katika gridi ya Taifa na Mtambo
mmoja wa kituo cha kinyerezi namba 2 Umekamilika na kuzalisha megawati 215 za
umeme.
Pia,TANESCO imesema imeshakamilisha matengenezo ya mtambo
mmoja wa kituo cha kidatu na kuanza kuzalisha megawati 50 za umeme katika gridi
ya Taifa kuanzia novembe 24 mwaka huu.
Hayo
yameelezwa leo Jijini Dar es Salaam na
Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO,Maharage Chande,wakati akizungumza na waandishi wa habari
wakati akitoa taarifa kuhusu Jitihada
zinazofanywa na shirika hilo kukabiliana na upungufu wa uzalishaji wa
umeme uliojitokeza kutokana na kuwepo kwa ukame.
Chande amesema
kutokana na matengenezo hayo kukamilika imepelekea kupungua kwa wastani wa kati
ya megawati 300 hadi 350 wiki iliyopita hadi kufikia megawati 215 za umeme wiki
hii
Aidha,Chande,amesema
mvua zilizonyesha maeneo mbalimbali nchini hazaweza kujaza kwenye mabwawa ya
kuzalisha umeme ya Pangani na Kihansi na kupelekea kuendelea kuwepo kwa
upungufu wa umeme kwenye gridi ya taifa.
Hata
hivyo,Chande,amesema iwapo mvua zitaendelea kunyesha katika mabwawa yote ya
kufua umeme na matengenezo yaliobaki kukamilika kama yalivyopangwa
yatasaidia kumalizika mgao wa umeme.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni