Zinazobamba

Tamasha Kubwa la Uimbaji na Miujiza Limeanza leo Jijini Dar es salaam

Mwinjilisti Dkt Piter Youngren (katikati) akifafanua jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari(hawapo pichani) jiji Dar e s salaam,kushoto kwake ni Askofu Mkuu wa BCIC Askofu Sylivester Gamanywa na kulia kwake ni Mkalimani wake.

Na Mussa Augustine.

Mwinjilisti wa Kimatiafa Kutoka Nchini CANADA Dkt Piter Youngren  amewasili nchini Tanzania kwa mara nyingine kwa ajili ya tamasha kubwa  la siku tatu la uimbaji na Miujiza litakalofanyika katika kanisa la BCIC Mbezi Beach Jijini Dar es salaam linalongozwa na Askofu Mkuu Sylvester Gamanywa.

Akizungumza mara baada ya kupokelewa Kanisani hapo Dkt Youngren amesema kuwa maombezi hayo yatalenga kuombea maisha ya Watanzania waliokumbwa na matatizo mbalimbali pamoja na kuliombea Taifa kutokana na kukumbwa na majanga mbalimbali yakiuchumi, Kisiasa na kijamii

 Dkt Youngren amesema kwamba maombi hayo ya siku tatu ambayo yameanza leo Desemba 2 hadi 4 yatasaidia kuwaondolea changamoto mbalimbali  Watanzania wenye changamoto mbalimbali ikiwemo  magonjwa,ukosefu wa Ajira,Ukraine pamoja na migogoro ya ndoa,inayowafanya  wakate tamaa katika maisha yao.

"Kila wakati wa majanga ni fursa, Ulimwengu unakabiliwa na majanga , Uchumi kuporomoka haya yanatufanya  sisi viongozi wa dini tufanye mambo mazuri zaidi katika maombezi yetu hivyo tunachohitaji ni ufahamu mpya katika wakati huu changamoto kwani ni mkakati za fursa " alisema Dkt Youngren.

Kwa Upande wake Askofu Mkuu wa  Kanisa la BCIC Askofu Silvester Gamanywa amesema kwamba wanatarajia mabadiliko makubwa yakiroho na kiuchumi kupitia tamasha hilo la uimbaji na miujiza hivyo ameiomba jamii kujitokeza kwa wingi kushiriki katika tamasha hilo.

"Maombi haya nikwa ajili ya kuombea Jamii na Taifa kwa ujumla , tunatarajia matokeo makubwa, nawaomba watu wenye matatizo mbalimbali waje wapate huduma ya maombezi katika tamasha hili la historia" alisisitiza Askofu Gamanywa.

 

 

Hakuna maoni