Wadau wa Mazingira kutoka Nchi Wanachama 15 wa Afrika Wameshiriki katika Mafunzo ya Utunzaji wa Mazingira ya Bahari
Wadau wa Mazingira
kutoka nchi wanachama 15 wa Afrika wameshiriki katika Mafunzo ya siku tatu kwa ajili
ya kukuza uelewa wa pamoja juu ya Mkataba wa kimataifa wa Utunzaji wa Mazingira
ya Bahari .
Akizungumza
wakati wa Mafunzo hayo Desemba 12 jijini Dar es Salaam Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (sekta ya uchukuzi) Dkt. Ally Possi amesema kuwa
Mwitikio wa nchi mwanachama umekuwa mkubwa na ni jambo ambalo dunia imeanza
kuipa kipaumbele Mkataba wa kimataifa kwaajili ya kulinda mazingira ya bahari
ili kuhakikisha viumbe vitakavyo zaliwa majini vinakuwa hai.
Akizungumzia
kuhusiana na Hali ya bahari kwa sasa amesema kuwa Mazingira ya Bahari kwa sasa
ni manzuri lakini tahadhari mbalimbali lazima zitolewa kwaajili ya Vizazi vya
vijavyo.
"Ifahamike
kuwa vyanzo vya maji hususani bahari vinasimamia sera ya uchumi wa bluu, sasa
bahari inapochafuka na inapoharibiwa kimazingira, sera ya uchumi wa bluu
inakuwa ngumu kwani kwa sababu ya viumbe ambavyo vinafanyika kuwa uchumi
vitapotea pamoja na vyombo vya usafiri majini vitaharibika na kushindwa kufanya
kazi inayotakiwa."amesema Dkt. Possi
Amesema kuwa
mkutano huo utatilia mkazo wa uridhiaji wa itifaki ya sheria ya bahari kwaajili
ya kuendeleza uelewa mpana wa wadau wote.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Kaimu Mkeyenge amesema Shirika hilo limekasimiwa mamlaka ya kudhibiti mazingira ya majini na Maji yanayotokana na uchafunzi wa vyombo vya Usafiri Majini hivyo madhumuni ya warsha hiyo ni uelewa wa pamoja wa Jinsi ya kudhibiti maji, kusimamia masuala ya usafiri majini.
"kwa
kukaa sana yale maji inawezekana kuna viumbe ambavyo vinazaliwa na yale maji
yaliyokuwa kwenye meli hakishushwa baharini katika maji ya kitaifa au eneo
lolote la bahari kunauwezekano wa kushushwa na viumbe wengine ambao wamezaliwa
baada ya yale maji kukaa muda mrefu,"Amesema Mkeyenge.
Nakuongeza
kuwa “Hivyo basi yale maji yakishushwa yanaweza kuzalisha viumbe wengine
ambavyo vitakuwa hatarishi kwa uendelevu viumbe ambao wapo baharini na
tunavihitaji.
Amesema
uchumi wa bluu unaweza usifikiwe kama maji yanakuwa hayadhibitiwi. Kwahiyo
hatutaufikia uchumi wa bluu kama mikataba hii hatutairidhia na kuzingatia ni
jinsi gani tunaweza kujikinga na hivyo viumbe ambavyo vinaweza kuzalishwa.
Shirika la Kimataifa la Bahari linatoa elimu kwa Taasisi mbalimbali zinazohusika na masuala ya usafiri kwa njia ya maji, taasisi zinazohusika na masuala ya bahari zimeshiriki mafunzo hayo ili kuwa na uelewa wa pamoja ili mkataba utakaporidhiwa na kutengeneza kanuni za Kutumika hapa nchini.
Kwa upande
wa Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira baharini kutoka Wizara ya Ujenzi na
uchukuzi, Sekta ya Uchukuzi Stela Katondo amesema kuwa maji yanahobebwa na meli
yanasaidia meli pale ambapo inakuwa haina mzigo pia ikiwa na mzigo mdogo
yanapunguzwa au kuongezwa ili kuweka uzito sawa katika meli na Maji hayo watu
wenye meli wamekuwa wakiyamwaga baharini jambo ambalo sio zuri.
"Maji
hayo yanaviumbe na mimea ambayo sio asili ya huku kwetu kwa hiyo ikitokea
yanamwagwa baharini yatakuwa na viumbe wavamizi wataleta namna tofauti ya
kimazingira Shirika la Kimataifa la Bahari (IMO) liliona umhimu wa kuweza
kudhibiti hali hiyo kwa sababu kimazingira sio sawa, kinachotakiwa ni kuto
kumwagwa baharini kama nchi mwanachama wa IMO tunatakiwa kuridhia mkataba huo
ili kuweza kusimamia kuwa haitakiwi ukifika bandarini kumwaga maji inatakiwa kwenda
kumwagwa katika kati ya habari ili yasiweze kuleta shida katika eneo letu la
mazingira ya maji.
Amesema Kwa Tanzania Sasaivi tupo katika hali nzuri kwa sababu tumeshaanza kuridhia mkataba pia amesema Kama wizara wameshatoa maoni na mapendekezo kwa wadau mbalimbali wanaohusika na mkataba huu. Na mpaka sasa wameshaanza kupokea maoni yao.
Washiriki wa Mafunzo hayo ni Wafanyakazi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Bandari, Taasisi ya Bahari ya Dar es Salaam (DMI) wa wawakilishi wa Nchi 15 za Afrika
Hakuna maoni
Chapisha Maoni