Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt Kedmon Mapana ambaye pia ni Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)
Na Mussa Augustine.
Kamati ya Mdundo wa Kitaifa
iliyoundwa hivi karibuni na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo
Mohamedi Mchengrwa imesema inaendelea na mchakato wa ukusanyaji wa maoni na
Vionjo kutoka katika mikoa ya Kanda zote
nchini ili kusaidia kupata Mdundo wa
Kitaifa utakaoutumika kama kitambulisho
cha taifa la Tanzania .
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es
Salaam na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt Kedmon Mapana ambaye pia ni Katibu
Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) wakati akitoa mrejesho wa kazi
iliyofanywa na kamati hiyo kwa muda wa miezi miwili tangu kuteuliwa kwake mwezi
Julai Mwaka huu.
Aidha Dkt.Mapana amesema kwamba miaka
mingi Wanamuziki wa Tanzania wamekuwa
wakitumia mdundo ambao hauna asili ya Kitanzania ikiwemo “Piano” hali
inayopelakea kukosa fursa ya kualikwa kwenye majukwaa ya muziki ya kimataifa .
"Wanamuziki wa Kitanzania
wamekuwa wakikosa kualikwa kwenye matamasha ya muziki kutoka mataifa ya
nje kutokana na nyimbo zao kukosa uhalisia wa mdundo wa asili kwani
nyimbo nyingi wameigia mindundo ya nchi za Mangharibi"alisema Dkt Mapana
Hata hivyo amesisitiza kuwa serikali inatarajia ndani
ya miezi miwili iwe imeshakusanya maoni ya Watanzania kutoka makabila
mbalimbali nchini huku wakishirikiana na kamati hiyo yenye wajumbe 13 ikiwemo
waandaaji,waimbaji nguli wa muziki hapa nchini ili kusaidia kufikia lengo lililokusudiwa la kutengeneza mdundo wa kitaifa.
Dkt Mapana amesema hatua hiyo
ya ukusanyaji maoni na vionjo inaelekea ukingoni ambapo hivi sasa wako mbioni kuhitimisha, nakwamba Midundo inaweza ikawa zaidi ya miwili ikitegemeana na maoni ya Watanzania kwani
kutumika kwakwe hakutokuwa na masharti mengi na itaruhusiwa kutumika ndani na nje ya Tanzania .
Naye Mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya
Mdundo wa Kitaifa ambaye pia ni Mtangazaji nguli wa TBC Manju wa Muziki Bw.Masoud Masoud amesema
Mdundo wa asili wa Kitaifa unaoandaliwa na Wizara ya Tamaduni,Sanaa na Michezo,
utasaidia kumtambilisha mwanamuziki wa Kitanzania popote anapokwenda na
kupata fursa zinazotokea ambazo zilikuwa zinawapita kutokana na kuiga Midundo
ya mataiafa mengine .
" Hii inasaidia Wanamuziki wa
Kitanzania kutambulika kutokana na Mdundo wa asili wa Kitaifa, na baadhi ya
nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Burundi,Uganda,Kenya,Rwanda ha ta kule Nigeria
na Kongo wana Midundo yao ya Kitaifa ambayo inawasaidi kupata mialiko yakuenda
kushiriki kwenye majukwaa ya muziki katika mataifa ya ulaya na Marekani"
alisisitiza Masoud.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni