Zinazobamba

Taasisi ya HDT yaiomba Tanzania na Nchi zingine Barani Afrika Kuchangia Mfuko wa Global Fund


 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya HDT Dkt Piter  Bujari (katikati)akisoma tamko la Taasisi hiyo kuelekea siku ya uchangiaji wa mfuko wa Global Fund.

Na Mussa Augustine.

 Taasisi isiyo  ya kiserikali ya Health Promotion Tanzania ( HDT) imeiomba serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchangia Mfuko wa Global Fund kama nchi nyingine zilivyoweza kujitoa kuchangia.

 Ombi hilo limetolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo  Dkt Piter Bujari wakati akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es salaam kuelekea siku ya uchangiaji wa Mfuko huo utakaofanyika Septemba 19 hadi 21 mwaka huu nchini Marekani nakubainisha kuwa  wakati sasa umewadia  Tanzania iahidi kuchangia kiasi cha fedha kwenye Mfuko huo.

 Dkt Bujari amesema kwamba Mfuko huo ni mahususi kwa kupambana na Ukimwi,Kifua Kikuu na Malaria umeleta mafanikio makubwa Kwa nchi za Afrika ikiwemo Tanzania ,nakusisitiza kwamba licha ya kupata msaada wa kutoka kwenye Mfuko huo umefika wakati Tanzania na Nchi zingine za Afrika ambazo hazichangii Mfuko huo ziahidi kuchangia kwa awamu hii ya saba .

 Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Dkt Bujari inasema kuwa kwa Afrika pekee nchi kama South

Africa,Kenya,Benini,Namibia,Senegal,Lesotho,Cote D'Ivoire,Togo,na Zimbabwe,zimekua mstari wa mbele katika kuhakikisha nazo zinachangia Mfuko huo,pia hivi karibuni Uganda iliahidi kiasi Cha Dola za kimarekani milioni 6.

 Aidha kupitia taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa HDT Bujira imesema kuwa kidunia Mkutano Mkuu wa Uchangiaji wa Mfuko kwa awamu ya saba utafanyika nchini Marekani kuanzia tarehe 9 - 21 Septemba 2022 ,fedha hizi zinategemea kuokoa maisha ya wanadamu zaidi ya milioni 20 Duniani kote ifikapo mwaka 2026.

 "Kama ilivyotajwa hapo juu Kwa miaka mitatu 2024-2026 kiasi kinachohitajika ni Dola za kimarekani Bilioni 130 .2,ambapo Mfuko wa  Global Fund watachangia Dola za Marekani Bilioni 18 sawa na asilimi 14,vyanzo vya ndani Dola za Marekani bilioni 85.6 ,

 Wafadhiri mbalimbali wa Mfuko wa Global Fund wameahidi kiasi Cha Dola za kimarekani Bilioni 17 .5 ambapo mpaka sasa kiasi cha Dola za kimarekani Bilioni 16.6 zimeisha kusanywa kati ya dola za kimarekani Bilioni 18 sawa na asilimia 92 zinazohitajika." amesema Dkt Bujari.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya HDT Dkt Piter  Bujari(mwenye suti) akiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari huku wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali.

Aidha amesema kuwa kwa Muda mrefu serikali ya Tanzania imekuwa ikishirikiana na Mfuko wa kimataifa wa kupambana na Maradhi ya UKIMWI ,kifua Kikuu na Malaria katika kupanga na kutekeleza afua mbalimbali za kupambana na Maradhi hayo ambapo Global Fund ni Moja ya wafadhili wakubwa Duniani na Kwa nchi ya Tanzania katika kufikia malengo ya sasa ya kutokomeza maambukizi mapya ya kifua Kikuu na virusi vya UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

 Michango ya Global Fund imesaidia kupunguza maambukizi mapya,kuwapatia matibabu wagonjwa na hivyo kupunguza vifo na kuwawezesha wengi kushiriki shughuli za uzalishaji Mali na maendeleo ya nchi kwa ujumla hata hivyo ugonjwa wa kifua Kikuu umeendelea kuwa tishio kubwa nchini na Duniani kote ambapo vifo vitokanavyo na ugonjwa huo vimeongezeka Kwa mwaka 2020.

Hakuna maoni