Zinazobamba

Yanga yamsimamisha kazi anayedaiwa kuihujumu timu, ni wakili msomi Simon Patrick

 






Kaimu Katibu Mkuu wa mabingwa wa kihistoria hapa nchini, Dar es Salaam Young Africa (Yanga) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Sheria na Wanachama, wakili Simon Patrick hatimaye amesimamishwa kazi rasmi

Kwa mujibu wa taarifa iliyotangwa na Mwenyekiti wa Kalabu hiyo, Mshindo Msola, alisema sababu za kumsimamisha kuongozi huyo mwandamizi ni tuhuma za kuihujumu timu ya wananchi.

Maamuzi ya kusimamisha kazi Wakili msomi Simoni Patrick umefanywa na kamati tendaji ya klabu ya Yanga kupitia kikao chake walichofanya Novemba 17, 2020

Minong’ono ya wakili msomi Simon Patrick kutimuliwa Yanga ilianza kusikika toka wiki iliyopita lakini viongozi hawakuwa tayari kulitolea ufafanuzi suala hilo.

Kiongozi huyo anatajwa kuihujumu timu hiyo kwa kutoa siri na kuzipeleka kwa wapinzani wao jambo ambalo linaweza kukwamisha mikakati yao ya kutwaa ubingwa wa msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL).

Tetesi zinadai kuwa kuanzia sasa majukumu ya Wakili Patrick yatakuwa chini ya Mwenyekiti wa klabu hiyo Dkt. Mshindo Msolla.

Yanga wameamua kufikia maamuzi hayo baada ya kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji kilichokaa jana Novemba 17, 2020 ambacho kilifanyika maalum kwa ajili ya kusikiliza shutuma ambazo amehusishwa nazo.

Kwa dhumuni la kuhakikisha haki inatendeka, Kamati ya Utendaji itateua Kamati Huru kuchunguza swala hili na kutoa maamuzi yenye tija kwa pande zote.

Hivyo, Kamati ya Utendaji itaisubiri Kamati Huru kukamilisha uchunguzi wake na kutoa ripoti juu ya tuhuma hizi.

 

Hakuna maoni