Zinazobamba

Sahau kuhusu Chama kwenda klabu ya Yanga, anamkataba na simba kwa miaka miwili na nusu-Dewji

 



 

"Ukweli ni kuwa Chama tumeshaini nae mkataba atabaki na Simba hadi msimu wa 2022 kwahiyo ana msimu nusu na miaka miwili imebaki, mimi kama Mwenyekiti siwezi kuja hapa kuongea mambo ya uongo,"

Ni Kauli ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Simba, Mohammed Dewji wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata la kiungo Clatous Chama juu ya kubaki mitaa ya msimbazi.

Mohammed Dewji alisema kiungo, Clatous Chama amesaini mkataba mpya kusalia klabuni hapo hadi 2022 na kufuta tetesi kuwa huenda angeweza kuachana na miamba hiyo ya soka hapa Tanzania Mwishoni mwa msimu huu.

Alisema baada ya kuwepo maneno mengi kuhusiana na nyota huyo kuhusishwa na uhamisho wa kwenda Yanga wameamua kumuongezea mkataba.

Kwa upande wake chama ambaye yupo nchi kwao Zambia aliandika kupitia mtandao wake mananeno yakiashiria kuendelea kusalia samba.

 “Taarifa sijui anakwenda Yanga ni mambo ambayo si sahihi, hakuna sababu ya kuwa na hofu na ninawatoa hofu mashabiki wa Simba kuwa tuko makini sana.

“Sehemu mbalimbali zimekuwa nikikutana na mashabiki wa Simba ambao wananiambia Mo fanya Chama asiondoke Simba. Chama ni mchezaji wa Simba.

“Suala kwamba anakwenda Yanga sijui linatoka wapi lakini haina shida, sasa nimewaambia na ninafikiri leo tunafunga mjadala,” alisema Mo Dewji.

Siku za karibuni kumekuwa na ripoti mbalimbali zinazomhusisha Chama raia wa Zambia kuwa anamaliza mkataba wake mwezi Juni mwakani hivyo anaweza akatua sehemu yoyote kama mchezaji huru lakini kutokana na maneno ya Mo Dewji huenda tukaona Mwamba huyo wa Lusaka akiendelea kukitumikia kikosi cha Wekundu wa Msimbazi Simba.

 


Hakuna maoni