Zinazobamba

TECNO SMART HUB KUBWA ZAIDI KUZINDULIWA JUMAMOSI.

TECNO imeeendelea kuhakikisha wateja wake wanapata huduma bora Zaidi kuwahi kutokea katika biashara simu kwa kutengeneza duka jipya la kisasa zaidi.
 TECNO SMART HUB ndio jina  sahihi la maduka haya mapya yanayofunguliwa na kampuni hii, duka hili jipya la kisasa linatarajiwa kufunguliwa eneo la Mlimani city , jengo jipya ambapo kutakua na  watu maarufu mbalimbali walioalikwa , wadau wa kampuni ya TECNO pamoja na mashabiki wa TECNO mitandaoni.

 Duka hili kubwa linalotarajiwa kufunguliwa siku ya jumamosi maaraufu kama TECNO SMART HUB litakua linatoa huduma bora zadi ya maduka mengine ya kawaida  ya simu. Huduma zinazotarajiwa kutolewa katika TECNO SMART HUB ni pamoja na mauzo, huduma baada ya mauzo na kikubwa katika maduka haya elimu mahsusi juu ya matumizi ya simu janja  “smartphone” itakua inatolewa na wabobezi wa simu hizo watakao kua dukani muda wote, lakini pia wateja watkaohudumiwa katika duka hili  wataapta nasafi ya kupumzika na kupata vivywaji huku wakipata huduma bora.


TECNO SMART HUB itazinduliwa siku ya jumamosi tarehe 7 ambapo watu 200 wa kwanza kuingia dukani watapata zawadi za bure wakati kwa wanunuaji wa simu siku hiyo watakua na nafasi za kupata zawadi mbili kwa mpigo, furaha Zaidi ni pale ambapo wateja wote wataweza kuingia katika bahati  nasibu ya kushinda televishen ya inchi 32 mbili pamoja na zawadi zingine kama feni, power bank na majagi ya umeme.
Wakati wa uzinduzi wa duka hilo jipya, vinywaji baridi  vitakua vinatolewa kwa wateja  wa bidhaa mbalimbali zikiwemo hata vifaa vya simu  pamoja na siu zenyewe, kadi maalumu za matengenezo ya simu zitatolewa pia kwa  wateja “VIP card”, huku burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali zikitawala eneo hilo kuhakikisha TECNO SMARH HUB linakua sehemu ya kisasa Zaidi.

TECNO inawaalika  wateja wote kwenda kununua simu kattika  duka hili jipya la kisasa ili kujishindia zawadi mbalimbali na kuingia katika familia ya TECNO kupitia bidhaa zilizopo katika SMART HUB.