Zinazobamba

PIKIPIKI ZA KINGLION ZINAVYOTATUA TATIZO LA USAFIRI VIJIJINI



Na Magali
Afisa Mtendaji msaidizi wa Kampuni hiyo, Bw Arnold Lymo maarufu kama (Riziki) akionyesha baadhi ya pikipiki ambazo zinafanya vizuri huko vijijini
Ukizungumzia pikipiki zinazofanya vizuri  katika soko Tanzania, huwezikukosa  kutaja pikipiki za Kinglion, ni pikipiki ambazo katika kipindi kifupi zimeweza kuteka soko la vijijini na kutatua kabisa kero ambazo kwa hakika zilikuwa changamoto.
Iko hivi, pikipiki za Kinglion kwa sasa ndiyo zimeshika soko la Tanzania, ni pikipiki ambazo zimeanza kama “underdog” yaani siyo tishio lakini taratibu watanzania wameanza kuziamini na kuzimia kuliko pikipiki zingine zozote kwa sasa.
Huwezi kubisha… utafiti uliofanywa na mtandao wa Fullhabari Blog unaonyesha Pikipiki za Kinglion zimeweza kuenena kwa kasi ya kimbunga katika soko la Tanzania hussani maeneo ya vijinini, Wafanyabiashara wengi wamekuwa wakikimbilia pikipiki za Kinglion, ni aghalabu  sana kuzikuta pikipiki zingine maeneo ya vijijini…kila kona ya kijiji ni Kinglion!Kinglion!Kinglion.
Kufuatia hali hiyo…Fullhabari Blog ilimtafuta Afisa Mtendaji Msaidizi wa kampuni ya Kinglion Investment Co. Ltd ili kufahamu “siri” ya mafanikio hayo.
Akizungumza na Fullhabari. Blog Afisa Mtendaji msaidizi wa Kampuni hiyo, Bw Arnold Lymo maarufu kama (Riziki) amesema siri kubwa ya kampuni yao kukua kwa kasi hapa Tanzania ni kujitoa kwao kusaidia jamii ya Tanzania kwa kuuza bidhaa zao kwa bei ambayo ni rafiki lakini pia kutoa huduma bora  kwa kujibu mahitaji ya walaji.
Riziki amesema walijaribu kuliangalia soko kwa karibu na kujua jamii ya vijijini inasumbuka na matatizo ya usafiri…wananchi wanatumia muda mrefu kutembea ili kupata huduma… wengine inawachukua muda mrefu kubeba mizgo yao kufika majumbani kwao…tumeona hiyo ni fursa na kuamua kuja na muarobaini utakaotatua kero hizo.
Riziki anasema baada ya kuziona fursa hizo tukawa tunaagiza bidhaa kulingana na mahitaji ya Wateja wetu…
Amesema kwa vijijini wateja wengi walikuwa wanahitaji pikipiki ambazo zinaweza kubeba mizigo mizito na ambayo haiwezi kuharibika kwa haraka.
 Kufuatia hali hiyo Kampuni iliamua kujipanga na kuamua kuleta pikipiki kulingana na mahitaji jambo ambalo limesaidia kwa kiasi kikubwa kukua kwetu kwa haraka hadi kufikia kushika nafasi ya kwanza katika soko la Tanzania.
 “Watu wengi hawafahamu…Kampuni yetu ndiyo namba mona hapa nchini kwa sasa, lakini watu watakutajia  wengine sisi haitushi tunachojua ni kwamba tunafanya vizuri sokoni” Alisema Riziki.
Aidha akizungumzia mipango ya baadae…Riziki amesema wamejipanga kuhakikisha wanatoa huduma iliyo bora na itakayotatua changamoto za watu hususani huko vijijini.

Kama unavyoona tumekuja na bidhaa zingine mpya hapa katika maonesho….lengo letu ni kuwaonyesha watu nini tunafanya kuhakikisha huduma zinazotolewa ni bora…tunawahakikishia watanzania kuwa sisi tutaendelea kutoa huduma iliyo bora na ya kuaminika.
Kampuni ya Kinglion Toka kuanzishwa kwake tayali imefikisha miaka 10, na imeweza kuenea Nchi nzima na kwamba bidhaa zake zimendelea kuaminika na watanzania walio wengi.