Zinazobamba

LHRC YAKUMBUSHIA TEGETA ESCROW-; LUGUMI, RICHMOND NA UNUNUZI WA RADA...WAMUOMBA RAIS MAGUFULI KUCHUKUA HATUA DHIDI YA KASHFA HIZO

KITUO CHA SHERIA na haki za binadamu (LHRC) kimeikumbusha serikali kuhusu kuchukua hatua dhidi ya kashfa ambazo zimesababisha Serikali hasara ikiwamo kashfa ya ununuzi wa rada, kashfa inayohusishwa na Kampuni ya Lugumi, kashfa ya Richmond, kashfa ya uwepo wa harufu ya rushwa katika miradi mbalimbali inayotekelezwa na mifuko ya hifadhi ya jamii …mathalani mradi wa NSSF kigamboni pamoja na suala la Vitalu vya uwindaji na umiliki wake.