PROFESA LIPUMBA AWASHUKIA WANAOUBEZA MUUNGANO,PIA AMSIHI MAALIM SEIF KUREJEA OFISINI SOMA HAPO KUJUA
NA KAROLI VINSENT
WANACHAMA cha wananchi (CUF) wametakiwa kutoutumia
mgogoro unaoendelea ndani ya Chama hicho ili kuvunja muungano uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar.
Ushauri huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti
wa chama hicho ambaye anatambulika na
ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa nchini,Profesa Ibrahimu Lipumba wakati wa
mkutano na waandishi wa habari.
Ambapo Profesa Lipumba amesema inasikitisha kuona
wako baadhi ya viongozi wa chama hicho wanautumia mgogoro wa kikatiba
unaendelea ndani ya chama hicho ili kuharibu muungano uliopo jambo analodai
halifai kufanywa na viongozi wa chama hicho kikuu cha Upinzani visiwani
Zanzibar.
“Kukweli ukitoa Chama cha Mapinduzi (CCM) chama
kingine ambacho kinauenzi muungano ni Chama cha CUF,hivyo nashangaa wapo
viongozi wanaobeza muungano huu,hivyo lazima tuwapinge watu hawa’amesema
Profesa Lipumba.
Hata Hivyo,Lipumba ameendelea kumsihi katibu mkuu wa
Chama hicho,Maalim Seif kurejea ofisini ili waweze kukijenga chama hicho.
Amesema kitendo cha Katibu mkuu huyo kutokuja
ofisini kunazidi kiweka vibaya chama hicho na kushindwa kueleweka kwa jamii
jambo analomsihi katibu mkuu huyo kutafakari uamuzi wake wakutokuja ofisini