Zinazobamba

TAASISI YA TICHER JUCTION YAWAPIGA MSASA WALIMU,SOMA HAPO KUJUA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiTEvUy43lLfbQnMocVHLG04W3SwK0EbjmTM-o4ftv5ZHDV2gwbGULkkMbuTbxA7n2QfodsJVmJFTXoSwKOWIOiNRm5TrnMMjFhoI6Z-xylrDwwVYiGIz1WRjuH4Uf1Ts-Ws7q7e4pDuU0/s1600/DSC_1477.JPG
Walimu nchini wametakiwa kujitadhimini ili kujua mbinu za kufundishia ili waweze kuwapa mafunzo bora wanafunzi

Wito huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam,!Afisa Mradi wa Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya TicherJuction,Njama Salum wakati akitoa mafunzo kwa walimu mbali mbali nchini yenye lengo la kuwapa walimu mbinu za kufundishia pindi wawapo shuleni.Taasisí hiyo ambayo imekuwa ikihusika katika kuwajengea uwezo kwa walimu pindi wamalizapo vyuoni waweze kupata kazi.
Amesema licha ya walimu kumaliza vyuo mbali mbali,lakini bado walimu wamekosa mbinu ya kufundishia wanafunzi jambo analodai limepelekea waajiri kushíndwa kuajiri walimu hao.

Njama amezitaja mbinu hizo ni pale mwalimu kushindwa kuweza kusimama kwenye darasa wakati wa kufundisha ,pia   wengi wao kushindwa kutoa uwezo wake na kupeleka kwa mwanafunzi.
Amesema baada ya taasisi hiyo kubaini changamoto hizi kwa walimu ndio ikawafanya kuandaa mafunzo hao ili kuwakomboa walimu.
Hata hivyo,Njama ameitaka serikali itunge mtaala ulio sahihi ili kumfanya mwalimu aweze kupata ajira.