Zinazobamba

CHAMA CHA CUF CHALIA NA RAIS MAGUFULI,WADAI NDIO KIKWAZO CHA KUFANYA BIBAYA KWENYE UCHAGUZI MDOGO,SOMA HAPO KUJUA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjVFs9r0eNsoGSeppBCYbVsoVZZ-HESX8ME3wqpOSQH7JOEnV4EM4cMLSjfYcLHYqE6nxRdVTnjCcaHF1HaeABizG0URVtTCZx24FafAAbwNa4lp5cwrHB3zwjwHe7Sc8Cae8pzYe8Rst4R/s640/Abdul+Kambaya.jpg
NA KAROLI VINSENT
Chama cha Wananchí (CUF) kimesema  katazo  la Rais John Magufuli kutoruhusu mikutano ya siasa pamoja na Nguvu kubwa inayotumiwa na vyombo vya dola kwa vyama vya upinzani ndio  sababu iliyochangia chama hícho kufanya vibaya kwenye uchaguzi mdogo uliomalizika hivi karibuni .
Ambapo katika uchaguzi huo mdogo uliofanyika januari 22,Chama Cha Mapinduzi CCM kilishinda Kata 19 kati ya kata 20 za udiwani pamoja na kushinda jimbo moja Dimani ,huku Chama cha demokrasia Chadema kimeambulia kata moja huku chama cha Cuf hakijaambulia hata kata moja.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam,Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Cuf,Abduri Kambaya(Pichani),wakati akitoa tathmini ya uchaguzi huo,
Ambapo amesema kitendo cha Rais Magufuli kukataza mikutano hiyo kimekiathiri chama hicho,amedai kuwa  pindi walipokwenda kupiga kampeni kwenye kata hizo wameonekana wageni,
Amedai kuwa  Chama cha CCM kinatumia mwanya huo kushinda katika uchaguzi huo.
Mbali na sababu hiyo,pia Kambaya ameitaja sababu iliyopelekea chama hicho kufanya vibaya ni matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola kwa vyama vya upinzaní ikiwemo kuwakamata viogozi wake jambo lilowatisha wapiga kura