Zinazobamba

WANAHARAKATI WAIBUKA NA KUDAI KATIBA MPYA,THRDC WAKOLEZA MOTO,SOMA HAPO KUJUA



 thrdc
WAKATI Rais John Magufuli akisema serikali yake hataliweka kipaumbele zoezi la Katiba mpya kwa kile anachodai anataka kujenga nchi kwanza.

Nao Mtandao wa Haki za Binadamu Tanzania THRDC kwa kushirikiana na wadau wengine wa katiba nchini wameamka na kufufua upya mchakato  huo  ambapo kwa madai yao wamesema kuuwa mchakato ulisitishwa baada ya kutokea pande mbili zilizovutana yaani walioikubali na walioipinga katiba pendekezwa

Akizungumza na Waandishi wa Habari mwishoni mwa wiki Jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa mjadala wa kitaifa  kuhusu namna ya kufufua mchakato upya  Rais wa Chama cha Wafanyakazi Nchini TUCTA, Gratian Mukoba ameeleza  kuwa  ni muda muafaka kwa asasi za kiraia kubeba agenda mpya ya uandikwaji wa katiba bora ya Tanzania itakayolenga kuleta ustawi kwa Taifa na Wananchi kwa ujumla.

Aidha, Mukoba amefafanua kuwa ili wananchi waweze kujitokeza  kwa wingi kuipigia kura za maoni katiba pendekezwa, ni vyema muafaka wa kitaifa utawawezesha wananchi wote kuungana na kuwa na maamuzi yanayofanana yatakayowaongoza kwenye zoezi zima la upatikanaji wa katiba mpya ukapatikana kwani kwa kufanya hivyo kutaondoa uwepo wa makundi ambayo yanakinzana.