Zinazobamba

UKAME KUITIKISA NCHI TENA,TMA YATABILI HALI HIYO,SOMA HAPO KUJUA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgB0CrqEs7ili8a38VPPQAWNVKlq2LK18ir5iKktfMkrdFLhPVCXLyOoW_mqu4HKgIxixOZ5okQmNGt-ExEp93ZYouruuamxhP7W56hmowSvAdGP5T7MId8uojc8iAz7T-bZq1JjPl2Nrw/s640/agness-Kijazi.jpg
NA KAROLI VINSENT
MAMLAKA ya Hali ya hewa nchini (TMA) Itabili  hali ya ukame takribani mikoa yote kutokana na kutokuwapo na mvua katika mwezi huu Novemba.
Hata Hivyo,Maeneo ya mikoa ya Kanda ya ziwa pekee ndio yanatarajiwa kuwa na mvua kiasi.
Hayo yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa mkuu wa (TMA)Dkt Agnes Kijazi wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo amesema hali hiyo ya kutokuwa na mvua imetokana na upugufu mkubwa wa unyevunyevu unaonekana katika maeneo mengi ya nchi kutokana na kuendelea kuwepo kwa viashiria  vya kupunguza mvua.

“Tumeona Lanina  na joto la bahari la chini ya wastani katika eneo la magharibi mwa bahari ya Hindi ,na hii sababu ndio imechangia kuwpo kwa upungufu wa mvua katika maeneo mengi ya nchi “amesema Dkt Kijazi.
Hata Hivyo,Dkt Kijaza amewataka Wakulima pamoja na Wafugaji kujiandaa na hali hiyo kwa kuhakikisha wanatunza akiba ya maji iliyopo .
Amesema licha ya Utabili huo  kuonyesha kuwapo kwa mvua chache (chini ya wastani) kuna uwezekano wa matukio ya vipindi vya mvua kubwa  pia kunaweza kutokea.