MWIGULLU NCHEMBA AJITOSA KIPIGO CHA MWANAFUNZI MKOANI MBEYA,SOMA HAPO KUJUA

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ameagiza
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya kuwakamata walimu walioonekana kwenye video
wakimwadhibu mwanafunzi vibaya. Tukio hilo lilitokea 28. September.
==>Taarifa rasmi za Waziri wa
Mambo ya Ndani
Mnamo Tarehe 28.9.2016, mwanafunzi aitwaye Sebastian Chinguku wa form 3A mbeya day sec school aishie Uyole alipigwa na walimu watatu, Mwl Frank Msigwa, John Deo UDSM na Sanke Gwamaka wa Nyerere Memorial, wote wakiwa mafunzo.
Mnamo Tarehe 28.9.2016, mwanafunzi aitwaye Sebastian Chinguku wa form 3A mbeya day sec school aishie Uyole alipigwa na walimu watatu, Mwl Frank Msigwa, John Deo UDSM na Sanke Gwamaka wa Nyerere Memorial, wote wakiwa mafunzo.
Mwl Frank alitoa assignment ya Kingereza na baadhi ya wanafunzi hawakufanya akiwepo Sebastian , darasani mwl alimpiga kofi kijana na kijana akahoji kwanini anampiga wakashikana koo, ndipo walimu wakamchukua na kumpeleka staff room na kuanza kumpiga .
Tangu tar 29. September mwanafunzi hakuonekana shuleni. Na mwl E.H wa Iringa University ndio aliyekuwa akisema mwacheni mtamuumiza na ndiye aliyechukua video.
Hao walimu wote hawapo wameondoka kwenda kwenye vyuo vyao. POLISI wanaendelea kuwahoji uongozi wa Mbeya Day Sec School na Mwanafunzi aliyeumizwa ikiwepo kumpeleka hospitali.
Nimeelekeza vyombo vya dola Dar wawatafute chuoni kwao hao walimu kuhusiana na shambulio hilo kwa mwanafunzi huyo.