MAELFU WAMUAGA MUHAMMAD ALI...AMEACHA SOMO KUBWA
Maelfu ya watu wamehudhuria swala ya
Kiislamu ya kumuombea aliyekuwa mwanandondi bingwa duniani Muhammad Ali
ambaye alifariki wiki iliyopita.
Swala hiyo imefanyika katika ukumbi wa
‘Freedom Hall’ katika mji aliokulia wa Louisville huko Marekani siku ya
Alhamisi.
Waombolezaji walisikika wakimpa sifa Muhammad Ali kwa kuliita
jina lake wakati mwili wa bondia huyo ulipoingizwa ukumbiniViongozi wakubwa katika ulimwengu wa
ndondi na wanaharakati walikuwa sehemu ya waliohudhuria.
Swala
imeongozwa na Imam wa Alifornia, Sheikh Zaid Shakir, ambaye alikuwa
pembezoni mwa Muhammad Ali pindi alipokuwa anakata roho na kupata fursa
ya kumwombea dua ya mwisho kabla ya maziko
Itakumbukwa kuwa, Ukumbi wa Freedom Hall
ndio sehemu ambayo pambano la mwisho la Muhammad Ali lilifanyika.
Wakati huo huo , serikali ya Kongo Kinshasa imepanga kufanya sherehe
rasmi ya kumkumbuka mwanandodi huyu ambaye alipambana dhidi GEROGES
FOREMAN mwaka 1974, inchini humo kwa mwaliko wa aliyekuwa Rais wa nchi
hiyo Mobutu Seseko.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni