Zinazobamba

SERIKALI YAKANUSHA UPOTOSHAJI KUHUSU AJIRA ZA WALIMU,SOMA HAPO KUJUA

Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), imekanusha taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii kuwa imesitisha ajira za ualimu kwa mwaka wa fedha 2016/17.

Hivi karibuni taarifa hizo zilieleza kuwa  utafiti uliofanywa na Tamisemi umebaini kuwapo kwa ziada ya walimu 7,988 wa masomo ya sanaa na biashara hivyo haitaajiri walimu hao badala wataajiri wa masomo sayansi na hisabati.

Akizungumza na wanahabari  Katibu Mkuu wa Tamisemi, Mhandisi Mussa Iyombe amewataka wananchi kupuuza taarifa hizo kwani hazina ukweli wowote na zinalenga kugombanisha,kujenga chuki kati ya Serikali na walimu wa masomo hayo.

"Siyo kwamba ajira za walimu hakuna, ajira zipo. Ila wakati ukifika tutawangazia tunachosubiri sasa hivi suala la bajeti kuu liishe kwanza," amesema Mhandisi Iyombe.

Advertisement

Hakuna maoni