Zinazobamba

MADIWANI WA MANISPAA YA KINONDONI WAITILIA SHAKA SERA YA ELIMU BURE,SOMA HAPO KUJUA




Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob (katikati) akiongoza sala ya kufungua mkutano wa kwanza baada ya uchaguzi wa kumchagua Meya na Naibu Meya wa manispaa hiyo.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob (katikati) akiongoza sala ya kufungua mkutano wa baraza la Madiwani wa manispaa hiyo.

NA KAROLI VINSENT
MADIWANI  wa Manispaa ya Kinondoni wametilia shaka hatua ya serikali kutangaza elimu bure kwa madai kuwa kiasi cha fedha kinachotengwa kwenda kwenye shule kwa ajili ya kuhudumia sera hiyo ni kiasi  kidogo.

Madiwani hao bila kujaliitikadi zao za vyama, wameyasema hayo leo wakati wa kikao cha baraza la madiwani ya Halmashauri ya Kinondoni,

Eprahim Kinyafu  diwani wa kata ya Saranga kwa kiketi ya Chama cha Demokrasia Chadema amesema kiasi cha fedha cha Bilioni 4 zilizotengwa na Halmashauri hiyo kwa mwaka kwenda kusaidia elimu bure ni kiasi kidogo hakiwezi kukidhi mahitaji ya wanafunzi.

Amesema kiasi hicho kidogo kimewafanya walimu kushindwa kuwahaudumia wanafunzi huku akitolea mfano kiasi kidogo cha Laki tatu kinachotegwa kwa kila shule kwa ajili ya kuwalipa walinzi akisema 

Naye Diwani wa Kata ya Mwananyamala Songoro Mnyonge CCM amesema kuwa hadhani kuwa kwa kusema ukweli kama Magufuli atamtumbua ila akiweka itikadi yake pembeni, ufaulu wa wanafunzi utaporomoka sana kutokana na fedha hizo kuwa ndogo kiasi cha kuto kidhi mahitaji ya shule husika.

Imeelezwa kuwa kila mwezi Hazina hutuma shilingi 548 kwa kila mwanafunzi fedha ambayo pia haifiki kwa wakati shuleni na kufanya mahitaji ya mhimu kukosekana huku Raisi akisisitiza wazazi kutochangishwa.

Mahitaji mhimu kwenye shule ni chaki, posho za walinzi, maji kwa ajili ya matumizi ya vyoo, umeme, siteshenari, na vitu vingine.
Aidha imeelezwa kuwa kwa kawaida kila mwanafunzi anatakiwa kupata shilingi 10000 kwa mwaka lakini shuleni inafika shilingi 6000 tu huku shilingi 4000 ikienda TAMISEMI kwa ajili ya kununulia vitabu.
DiwaniMichael Urio wa Kunduchi alisema kuwa majibu toka kwa watendaji wa Halmashauri kila siku hayaridhishi na yamekinzana sana kutokana na usiri uliogubika fedha hizo na kuwataka watendaji hao kutoa taarifa ya fedha hizo kila mara kwenye vikao vya Baraza hilo.
“Majibu hayo mkurugenzi hayaridhishi kutokana na tarifa zake kugubikwa na usiri mkubwa tunaomba kuanzia sasa tuwe tunapewa kila mara ili tukienda kukagua huko mashuleni tuweze kusimamia” alisema Urio.
Aidha madiwani hao wameeleza kuwa shule nyingi katika Manispaa ya Kinondoni zinakabiliwa na uhaba wa vyoo na nyingine zimeshafungwa katika Kata ya Makuburi kutokana na uhaba wa matundu ya vyoo na wananshangaa Serikali inaangalia madawati tu.
Pia imeelezwa kuwa kuna baadhi ya Shule madasa hayana milango na nyingine katika Kata ya Goba hazina madarasa na hivyo kufanya wanafunzi kusoma wakiwa chini ya Mwembe.
MIUNDOMBINU
Katika hali nyingine, Madiwani hao wameonyesha kutokuwa kuwa imani na wakandarasi kutokana na barabara nyingi kujengwa chini ya kiwango huku wakilipwa fedha zote za miradi.
Songoro Mnyonge anasema katika Kata yake kuna Barabara inamiaka sita sasa ya urefu wa mita 800 hadi sasa haijakamilika huku wananchi wakiwa hawajui kwa nini mkandarasi huyo hamali ujenzi wa barabara hiyo.
Naye Kinyafu Diwani wa Saranga anasema kuna barabara ya kilomita 7 inayounganisha kata ya Saranga na Kimara mkandarasi  hajamaliza mpaka na ameitelekeza barabara hiyo huku akiwa amelipwa fedha zote mil 400.
“Ninashindwa kuelewa mhandisi wa wilaya aliyemleta mkandalasi Yule ana akili timamu au hajasoma, amemleta mkandarasi bila taarifa kwenye Serikali ya Mtaa wala Ofisi ya Kata, sasa mkandalasi anapita vichochoroni baada ya kuharibu” alisema Kinyafu.
AFYA
Katika sekta ya Afya, Halmashauri imesema inajumlanya vituo vya Afya 25 huku vituo vinne vya Magomeni, Sinza, Mwananyamara na Boko vikiwa na magari ya kubebea wagonjwa na imetenga fedha za kugharimia wagonjwa akina mama katika vituovisivyo na magari na kusisitiza kuwa wagonjwa hawatakiwi kulipa gharama hizo.
Aidha wamesema kuwa wanajiandaa kufanya upanuzi wa vituo vilivyopo kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Mwanyamala.

Hakuna maoni