Zinazobamba

HOSPITALI YA AGA KHAN YAISHAURI SERIKALI,NI KUHUSU WAUGUZI,SOMA HAPO KUJUA





NA KAROLI VINSENT
SERIKALI nchini imetakiwa kuongeza wahudumu wa afya wakiwemo Wauguzi na Madaktari katika Hospitali zote nchini ili kuondokana na tatizo la wauguzi kuwahudumu wagonjwa wengi kuriko idadi ambayo Wauguzi wanatakiwa kuwahudumu.

Hayo yamesemwa  na Lucy Hwai ambaye ni Mkurugenzi wa Wauguzi  katika Hospitali ya Aga Khan nchini, wakati wa Maazimisho ya siku ya Wauguzi Dunia ambapo Hospitali hiyo nayo iliadhimishwa siku hiyo,

Ambapo Amesema kwa sasa Fani ya Wauguzi nchini inakumbana na Changamoto kubwa ikiwemo wauguzi kuwahudumia wagonjwa wengi kuriko idadi inayotakiwa.

Amesema kwa mujibu wa shirika la Afya la Dunia (WHO)  linatoa mwongozo kwa wauguzi kuwahudumu wagonjwa watano kila siku,lakini amedai kwa watanzania imekuwa ikikwenda kinyume ambapo Muuguzi mmoja anasimamia wagonjwa zaidi ya 60 jambo analodai linachangia kurudisha nyuma sekta ya afya.

Amesema kwa Sasa Serikali inatakiwa kuliwekea mkazo suala la wauguzi ikiwemo kuwekea mazingira rafiki katika Hospitali zote nchini hususani zilizopo Vijijini ili wauguzi hao wafanye kazi kwa umakini zaidi ili kuondokana na tatizo la Vifo vinavyotokana na kusababishwa na mazingira mabovu ya Wauguzi.

Hakuna maoni