Zinazobamba

BARAZA LA WAZEE LA YANGA LAIKOMALIA TFF NA BMT,SOMA HAPO KUJUA





BARAZA la Wazee la Klabu ya soka ya Yanga limelitaka shirikisho la Soka  nchini (TFF) pamoja na Baraza la michezo nchini (BMT) kutoa ufafanuzi wa haraka kuhusu kadi gani hasa zitumike na wanachama wakati wa kupiga kura kwenye uchaguzi wa Klabu hiyo .,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Ombo hilo limetolewa na Katibu mkuu wa Baraza hilo,Ibrahimu Akilimali wakati akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam, amesema Wazee hao wameshtushwa na Tamko lilotolewa na Tff pamoja BMT linalowataka wanachama wa Yanga wanaorusiwa kupiga kura kwenye uchaguzi huo ni wale tu wenye kadi  za zamani za Yanga na sio vingenevyo.

Amesema Tamko hilo linawapa shida wanachama kwa madai kuwa kwa sasa hivi wapo wanachama wenye kadi za Posta ,kutokana na wanachama wengi wa kadi za zamani wamebadilisha kadi zao na kwenda kwenye kadi za Posta.

Mzee Akilimali amebainisha kuwa kitendo cha kuwabagua wale wenye kadi za zamani   ndio wapewa haki ya kupiga kura na kuwaacha wenye kadi za Posta ni kitendo ambacho wanadi kuwa kitaleta mgogoro mkubwa  katika Klabu hiyo ambayo ni Mabingwa wa Kombe la Ligi.
Amesema kitendo cha kuwaruhusu wanachama wenye kadi mbili kupiga kura sio kitu kigeni kwenye Klabu hiyo  huku akitolea mfano uchaguzi wa mwaka 2006 kwa Yanga asili na Yanga Kampuni walivyotoa uongoa harali.
Hata Hivyo,Akilimali ameliomba BMT pamoja TFF kuiruhusu sekretarieti ya Yanga kuitisha mkutano mkuu wa Dharula  wa wanachama ambao utakuwa na ajenda ya Uchaguzi mkuu ili wanachama wapewe taarifa kuhusu uchaguzi.

Hakuna maoni