Zinazobamba

IGP MWEMA AMEKWISHA,KASHFA YA UFISADI WA LUGUMI KUMMALIZA,WABUNGE WAJIAPIZA,SOMA HAPO KUJUA





Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi Said Mwema

Ni Mungu tu ndiye atayeweza mwokoa alikuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini,IGP Said Mwema  kwenye Kashfa ya fisadi katika mkataba kati ya Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd na Jeshi la Polisi ndivyo naweza kusema  kutokana kutajwa kuhusika kwake.(Mtandao huu umedokweza).Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ambapo Kamati hiyo ilikuwa na kazi moja tu,ya kuchunguza Kampuni hiyo ambapo kwa sasa kazi ya uchuguzi huo umekamilika kwenye mikoa tofauti nchini na kinachosubiliwa ni kukabidhi ripoti hiyo kwa Spika ili isomwe kwa wabunge, 

Ambao chanzo chetu hicho kimeiambia Fullhabari.blogs kuwa  Kamati hiyo imebaini madudu ambayo yanamweka pabaya IGP Mwema.

“Ninachokwambia Ndugu,yaani tumebaini madudu mengi,ambayo kama wabunge wa CCM wakiacha mtindo wao wakukitetea chama basi,huyu IGP Mwema achomoki,kwasababu ni mtu ambaye anatakiwa kuchunguzwa mara moja na taasisi za kuzuia rushwa kama TAKUKURU,”Kimesema Chanzo chetu hicho.

Ametaja kinachomweka Pabaya IGP Mwema ambaye wakati mkataba wa Lugumi unaingiwa alikuwa IGP  ni kitendo chake cha kuhusika au kuwanyamazia viongozi wandamizi wa Jeshi la Polisi mpaka kupa tenda Kamapuni ya Lugumi kwenye Mkataba wa Bilioni 39 huku ikiwa haina sifa wala mtaji wa kuweza kutekeleza kazi hiyo.

“Yaani hii kampuni inautata sana,tumeibani kuwa haina sifa hata moja,harafu katika uingiaji wake mkataba na jeshi la Polisi inatokana shinikizo la huyu bwana (Mwema),kwa vyovyote vile kamati hii ikisomwa kwa wabunge nakuhakikishia utasikia makubwa na tumeapa kupambana mpaka haki itendeke,tumechoka kusikia tunatoa mapendekezo kama kwenye Escrow harafu tunapuuzwa,kwa sasa hatutakubali “kimezidi sema Chanzo chetu hicho.

Kuibuka kwa taarifa hii kuna kuja ikiwa wiki mbili baada ya Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA) Godbless  Lema wakati akiwasilisha maoni ya Kambi ya Upinzani Bungeni kwenye  Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambapo Mbunge huyo alisema Kampuni ya Lugumi imepewa tenda huku ikiwa haina sifa pamoja na kujaa upendelea mtupu wakati utoaji tenda.

  UTATA WA KAMPUNI YA LUGUMI.
Kampuni ya Lugumi inadaiwa kupewa tenda na jeshi hilo kwa ajili ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole – ‘Biometric Access’ katika vituo 108 nchi nzima kwa gharama ya Sh bilioni 37.

Hadi sasa mashine hizo zimefungwa katika vituo 14 pekee na tayari kampuni hiyo imelipwa Sh bilioni 34 ambazo ni sawa na asilimia 99 ya fedha zote za mkataba.

Katika sakata hilo, inadaiwa Kampuni ya Lugumi ilipewa zabuni hiyo ikiwa haina uzoefu wa kazi hiyo.

“Wamepewa mkataba sawa, lakini mbona taarifa zinaonyesha kuwa kampuni hii haijasajiliwa kama Biometric Access Company na haijawahi kufanya kazi zozote zinazohusu Biometric Access Control?” alihoji mmoja wa wataalamu.


Hakuna maoni