Zinazobamba

WAZIRI WA UJENZI AIAGIZA MAMLAKA YA HALI YA HEWA KUTEKELEZA HAYA, ASEMA WASIPOWAJIBIKA YATAWAFIKA YA TPA


Waziri wa Ujenz, uchukuzi na Mawasiliano Prof Makame Mbarawa ameiagiza mamlaka ya hali ya hewa hapa nchini (TMA) kuanza zoezi la kuweka utaratibu wa kupimana kuhusu utendaji kazi katika kila idara ili kuifanya mamlaka hiyo kuongeza ufanisi wake.
Akizungumza na wafanyakazi wa taasisi hiyo, mara baada ya kutembelea idara mbalimbali ya mamlaka hiyo,Prof. Mbarawa amesema kuna haja ya Mamlaka hiyo kuanza utaratibu wa kupimana
Alisema kufanya hivyo kutaongeza uwazi katika majukumu yao, kutawasaidia wafanyakazi kupandishwa madaraja na pia kutakuwa hakuna minong’ono ya upendeleo katika suala zima la kupandisha vyeo wafanyakazi.

“Naamini mamlaka hii inawanasayansi na wanafanya kazi zao vizuri, lakini nataka mjue sasa katika utawala huu mpya tunataraji kuanza kuweka utaratibu wa namna ya kutimiza malengo ya kutoa taarifa muhimu za kitabiri, mimi nitamuakiza mwenyekiti kutimiza hilo”
Katika hatua nyingine Prof Mbarawa ameitaka taasisi hiyo kuanza kuipa kipaumbele matumizi ya kidigitari na kuachana kabisa na matumizi ya makaratasi kwani sasa dunia inapoelekea inakimbilia katika kuachana na matumizi ya makaratasi na hivyo kupunguza gharama kwa serikali.

Hatua hiyo imekuja baada ya Waziri huyo kupita katika idara moja na kukuta taarifa nyingi zikihifadhiwa kwa mfumo wa mafaili, jambo ambalo amesema si sahihi na kuwataka wabadilike.

“Wakati napita kukagua ofisi yenu nimefika sehemu moja nimeona matumizi ya makaratasi ni makubwa, si vibaya lakini sasa tunapaswa kubadilika, tunauwezo wa kutunza taarifa hizo kidigitari, nitazungumza na watu wa Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) wawape mafunzo”Alisema

AKAGUA MRADI WA UPANUZI WA BARABARA YA MWENGE HADI MOROCCO
Katika hatua nyingine Waziri huyo  amekagua  mradi wa upanuzi wa barabara ya Mwenge  hadi Morocco yenye kilomita 4.3 ambapo ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 95.
Akizungumza na waandishi wa habari  leo jijini Dar es Salaam wakati wa ukaguzi huo Prof.Mbarawa ameeleza kuwa tayari njia tano zimeanza kutumika kuanzia eneo la Mwenge hadi Kijitonyama zenye urefu wa  kilomita 2 huku kilomita nyingine 2.3 zikiwa katika harakati za mwisho za kukamilishwa.
“Serikali imedhamiria katika kuhakikisha kuwa  inatatua kero ya  msongamano wa magari kwa kufanya upanuzi wa njia  muhimu ili kurahisisha hali ya usafiri jijini Dar es Salaam ” alisema Prof.Mbarawa.
 Aliongeza kwa kusema hivi karibuni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli alizindua mradi wa daraja la Kigamboni linalounganisha kurasini na Kigamboni pamoja na kuweka  jiwe la msingi  kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa  flyover katika eneo la Tazara .
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi.Patrick Mfugale ameeleza kuwa  mradi huo umekabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo uhamishaji wa mabomba ya maji safi na maji taka katika eneo la Makumbusho na Mwenge ili kuendelea na ujenzi.
Novemba 30 mwaka jana  Rais John Magufuli aliagiza kiasi cha shilingi bilioni nne kilichopangwa kutumika katika shamrashamra za siku ya Uhuru kitumike katika kazi ya upanuzi wa barabara ya Mwenge hadi Morocco jijini Dar es salaam yenye urefu wa kilometa 4.3 ili kuiunganisha barabara hiyo na ile ya Mwenge – Tegeta yenye urefu wa KM 12 .

Hakuna maoni