Zinazobamba

WAFANYABIASHARA SOKO LA NDIZI MABIBO SASA WAMVAA MEYA WA KINONDONI,



 
Kitambale(aliyeinua Mkungu akimuonyesha mpiga picha ndizi bora)
Soko la ndizi mabibo limekuwa ni maarufu sana katika jiji la Daresalaam, wengi wanalifahamu kutokana na umaarufu wake wa kuweza kurisha wakazi wa jiji la Daresalaam bidhaa ya ndizi kwa manispaa zote za Jiji .

Ni soko ambalo ndizi zote kutoka mikoa mbalimbali ya nchi ya Tanzania zinapokelewa hapo na kusambazwa katika masoko mengine ya Jiji .
Masoko ya Buguruni, Tandale, Ilala, Mwananyamala,sterio kule Temeke yamekuwa yakipokea bidhaa ya ndizi kutoka soko hilo la Ndizi Mabibo.
Soko hilo linahistoria ndefu, toka enzi hizo likiitwa soko la urafiki na baadae wafanyabiashara kuhamia eneo jipya ya Mahakama ya ndizi.
Kutokana na umuhimu wake,wakazi wa Jiji hilo wamekuwa wakifurika usiku na mchana kujipatia bidhaa ya ndizi tayari kwa matumizi mbalimbali.
Fullhabari ilipata fursa ya kuzungunmza na wafanyabiashara wa soko hilo kufuatia tetesi zilizopo kuwa soko hilo kwa sasa wafanyabiashara wake wamekuwa wakifanya biashara kwa hofu.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mmoja wa wafanyabiashara hao Bw. Amosi Pengo amesema kwa muda mrefu wamekuwa wakitoa kilio chao kwa viongozi wakuu wa halmashauri lakini hakuna majibu ya kuridhisha dhidi ya wasiwasi wao.
Mjasiliamali akihesabu mapato yake

Amesema kilio chao kikubwa ni kutaka kurasimisha soko hilo kuwa soko kamili na hivyo kodi inayotolewa na wananchi wa soko hilo iweze kuingia moja kwa moja katika serikali,
Akizungumzia athari wanayopata kutokana na soko hilo kutorasimisha kamili, Amesema wamekuwa hawana uhuru wa kufanya biashara zao kwa hofu kuwa muda wowote soko hilo linaweza kufutwa.
Amesema licha ya soko hilo kukusanya mamilioni ya shilingi kwa njia ya kodi wanazotozwa kila mwezi, hawaoni manufaa yake kwani hakuna huduma stahili zinazotolewa
 Amesema inawezekana kabisa fedha hizo zinaingia mifuko ya watu wachache na kushauri serikali kuangalia suala hilo.
“Tunadhani Dar es salaam ya Makonda inahimiza usafi, lakini hebu angalia soko hili limekuwa chafu kiasi ambacho wateja wamekuwa wakiteseka kupata huduma, tunashangaa kwanini haya yote yanatokea wakati kodi inalipwa” alihoji Mapengohali.

Akizungumzia hofu ya wafanyabiashara wa soko hilo, Amosi amesema watu katika soko hilo hawana Amani kabisa na kuendelea kufanya biashara hapo badala yake wamekuwa wakiishi kwa matumaini.
Katika hatua nyingine wafanyabiashara hao wamemuomba Meya wa manispaa ya Kinondoni Bw Boniface Jacob kuingilia kati na kulifanya soko hilo kuwa mikononi mwa serikali badala ya kuendelea kumilikiwa na kiwanda cha urafiki.
“Sisi Wafanyabiashara wa soko la ndizi mabibo urafiki jijini Dar es salaam tunaiomba serikali kuharakisha ombi letu la muda mrefu la kubadili eneo hili la soko kutoka kwenye kuendelea kuwa eneo la viwanda na kuwa eneo la soko rasmi ili tuweze kufanya biashara zetu kwa uhakika ikiwa ni pamoja na kukopesheka na kufadhiliwa” walisema
Kama unavyoona hapa ndipo Ndizi kutoka kila mkoa wa Tanzania hushwa kwa ajili ya kusambazwa kila pembe ya Dar es  lakini tumekuwa hatuthaminiwi kutokana na soko kumilikiwa na kiwanda.

Hakuna maoni