MAMBO YANAZIDI KUWA MAZURI KWA UKAWA,SASA WAPATA NAIBU MEYA JIJI LA DAR,SOMA HAPO KUJU
HATIMAYE uchuguzi wa
Naibu meya wa Jiji la Dar es Salaam ambao ulikuwa unasubiriwa
umemalizika na Mussa Kafana ametengazwa kuwa mshindi wa nafasi hiyo.Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo
Kafana
ambaye ni Diwani wa Kata ya Kiwalani jijini hapa kupitia Chama cha
Wananchi (CUF) ameibuka kuwa mshindi kwa kupata kura 10 akimshinda mpinzani wake kutoka Chama cha
Mapinduzi (CCM),Mariam Lurida ambaye alipata kura 6,
Uchaguzi huo ambao umefanyika leo mapema unakuwa
umekamlisha chaguzi zote za nafasi za umeya ambazo zilikuwa zinahairishwa mara kwa
mara.
Akizunguma mara baada ya kutawazwa kuwa Naibu
meya,Kafana amewataka Madiwani wote wa jiji na wabunge kuondoa itikadi zao za
chama kwa kujiingiza katika mipango ya kuwatumikia wananchi.
Khafani ambaye anaungwa mkono na Vyama vinavyounda
umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) amesema kwa sasa Wakazi wa Dar es Salaam
wategemee kasi ya maendeleo ambayo
ameifananisha kasi hiyo na Kasi aliyokuwa
nayo Rais Jamhuri wa Muungano wa Tanzania,John Magufuli katika kuwatumikia
wananchi.
Kwa upande wake Mbunge wa Ubungo,Saed Kubenea ambaye
naye ni mjumbe katika Baraza la Madiwani ammetaka Meya huyo kuhakikisha anakuwa
katika mstari mbele kuondoa mikataba yote anayodai ni ya kifisadi.
Kubenea ameitaja mikataba hiyo ni mikataba ya
Machinga Complex,tozo za kupaki magari.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni