Zinazobamba

CUF WACHACHAMAA NA SERIKALI YA RAIS MAGUFULI,WAIBUKA NA KUSEMA HAYA,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chama cha Wananchi (CUF) Abdul Kambaya akizunguma na Waandishi wa Habari leo Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho yaliopo Jijini Dar es Salaam,


NA KAROLI VINSENT
WAKATI ikiwa Vyombo ya Habari vya binafsi pamoja na Serikali kuzuiliwa kuonesha  mikutano ya Bunge la jamhuri wa Muungano  wa Tanzania Live (moja kwa moja,)

Wadau mbali mbali wamendelea kukosoa hatua hiyo kwa kusema serikali yeyote ya hovyo na isiyojihamini ndio inataka Bunge hilo kutorushwa moja kwa moja kwa kile kinachoitwa ni kitendo cha  serikali kuficha matendo ya maovu yasijulikane kwa wananchi.

 Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chama cha Wananchi (CUF) Abdul Kambaya, ambapo katika kikao Mkutano wake na Waandishi wa Habari,makao mkuu ya Chama hicho leo jijini Dar es Salaam,amesema kitendo cha serikali ya Rais John Magufuli kukataza Bunge lisionyeshwe ni wazi kuwa serikali hiyo imeanza kuongoza nchi Kidikteta.

Amesema Dalili za utawala wa Rais Magufuli za kubana uhuru wa habari zilianza mapema pale ambapo Waziri wa Habari,utamaduni,sanaa na michezo,Nape Nnauye alipolifungia Gazeti la Mawio na baadae Waziri huyo akazuia Bunge lisirushwe Live (Moja kwa Moja),
“Ni wazi Serikali hii umekuwa ni ya Kidiktea ambayo haitaki kuambiwa ukweli,na imeanza kuvunja katiba ya nchi ambayo inataka Mwananchi kupata taarifa,lakini leo serikali hii ya Magufuli imewazuia wananchi wasipate haki yao ya msingi ya kuonyeshwa kwa bunge moja moja”amesema Kambaya.
Kambaya ameeleza kuwa bunge likirushwa moja kwa moja linaongeza uwajibikaji, uwazi hivyo kutolionesha moja kwa moja ni kinyume na sheria ya Uhuru wa Habari kifungu cha 18 katiba ya mwaka 1977.
Naibu Mkurugenzi huyo amesikitishwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuvinyima uhuru vyombo binafsi vya habari katika kuripoti habari za bunge kwani ameseme kuwa Bunge limeanzisha kituo chake cha kurusha matangazo ambapo wanahabari watakuwa wanapatiwa habari na chombo hicho, pia hairuhusiwi kwa muandishi kuingia na kamera au kinasa sauti bungeni jambo ambalo amelifananisha na udikteta.
Kutokana na hayo yote Naibu Mkurugenzi wa Habari Kambaya amesema kuwa chama chake cha CUF kipo tayari kushirikiana na vyombo vya habari binafsi kupambana kufanikisha kuwa Uhuru wa vyombo vya habai unapatikana kwani sababu ya gharama za uendeshaji sio sababu ya msingi kwani luninga ya Taifa inapata ruzuku ya serikali inayotokana na kodi za wananchi, hivyo isiwe kisingizio cha kuwaficha wananchi ili madudu ya serikali yapite bila kupingwa

Hakuna maoni