Zinazobamba

JESHI LA POLISI NCHINI LAKITHIRI UVUNJIFU WA HAKI ZA BINADAMU,SOMA HAPO KUJUA


Jeshi la Polisi likifanya utesaji kwa raia



JESHI la Polisi nchini limetajwa kuwa kinara wa ukiukwaji wa haki za Binadamu kwa raia,kutokana na kukithiri vitendo vyake vya  kutesa raia pindi inapowatia hatiani.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Hayo yamesemwa leo na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora ,Dkt.Kevin Mandopi wakati kuadhimisha siku ya  Afrika ya kuzinduliwa kwa muongozo wa Luanda kuhusu haki za watuhumiwa wa makosa ya Jinai,wanapokamatwa na kuzuiliwa mahabusu kabla ya kushtakiwa,

Amesema kwa mujibu wa taarifa mbali mbali za tume hiyo,pamoja na malalamiko yanayopokelewa na tume kutoka kwa wananchi dhidi ya jeshi la polisi ni zaidi ya asilimia 60 ya malalamiko yanaelekwa kwa jeshi la Polisi kwa kukiuka haki za binadamu.

Amesema licha sheria ya Jeshi la Polisi ya mwaka 2002 kifungu cha 27 (3) kuwapa mamlaka polisi kumkamata mtu yeyote  iwapo kunasababu za sheria kufanya hivyo lakini amedai jeshi limetumia sheria hiyo kufanya uvunjifu wa haki za Binadamu. 

Dkt Mandopi ametaja uvunjifu huo wa haki za badamu unaofanywa na jeshi la Polisi ni kupigwa kwa Raia pindi wanapokamatwa,kutofikishwa Mahakamani kwa kubabikiziwa kesi,kunyimwa dhamana kutofikishwa mahakamani kwa wakati yanahusu kupigwa,kuteswa pamoja na kucheleweshwa kwa upelelezi.
Dkt Mandopi amesema mambo hayo  ni kinyume na matakwa ya muongozo wa Luanda,katiba,sheria za nchi,mikataba ya kikanda na kimataifa ya haki za bindamu.

Hata hivyo,Dkt Mandopi amesema kutokana hali hiyo  Tume za Haki za Binadamu na utawala Bora,Chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) pamoja na Jukwaa la Haki na usalama wameliomba jeshi la Polisi na taasisi za serikali kusimamia utekelezaji wa mchakato wa jina ikiwemo kuzingatia muungozo wa kimataifa ili kuliondoa taifa kwenye kazia hiyo


Hakuna maoni