UGONJWA WA SICKLE CELL WAIVURUGA SERIKALI,SOMA HAPO KUJUA
Pichani ni Yasmini Razak, mzazi wa Ronald Massamba ambaye
anasumbuliwa na selimundu leo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)
BAADA
ya kusitishwa utolewaji huduma ya bure kwa wagonjwa wa Selimundu (Sickle Cell)
katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), kumetokea mvutano baina ya wazazi wa
wagonjwa na uongozi wa hospitali hiyo, anaandika Regina Mkonde.
Mvutano
huo umechipuka baada ya Shirika la Trust Fund la nchini Uingereza kumaliza
mkataba wake wa mradi wa utafiti kwa watu wenye ugonjwa wa selimundu nchini
mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu na kwamba, mradi huo ulisaidia
wagonjwa
hao kupata matibabu bure kwa kipindi cha miaka 10.
Wakizungumza
kwa wakati tofauti leo, viongozi wa MNH na wazazi wa wagonjwa wametoa kauli za
mvutano ambapo wazazi wanataka huduma hiyo iendelee kutolewa bure huku uongozi
wa MNH ukisema kuwa, muda wa utolewaji huduma hiyo bure umeisha hivyo huduma
hiyo ni ya malipo.
Akizungumza
na waandishi wa habari Yasmini Razak, mzazi wa Ronald Massamba ambaye
anasumbuliwa na selimundu leo jijini Dar es Salaam amesema, baada ya kusitishwa
utolewaji huduma bure kwa wagonjwa, alifanya jitihada za kuomba msaada kwa
baadhi ya viongozi wa serikali ili huduma hiyo itolewe bure bila ya kufanikiwa.
“Nilipokwenda
Muhimbili kwa lengo la kumpeleka mwanangu kliniki, nikakuta huduma inayotolewa
ni ya malipo huku baadhi ya wazazi wenye wagonjwa wakilalamika juu ya gharama
wanazotozwa. Wengi wao hawakuwa na uwezo wa kulipia gharama hizo,” amesema.
Anaeleza,
aliamua kumtafuta Lawrence Museru, Mkurugenzi wa MNH baada ya kukosa
ushirikiano wake akamtafuta Grace Magembe, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
na kukosa msaada ndipo alipoamua kumtafuta Hamisi
Kigwangalla,
Naibu Waziri wa Afya ambaye pia alimuahidi kumsaidia ambapo mpaka sasa hajapata
msaada huo.
Razak
amesema, serikali haina budi kuchukua hatua mapema kusaidia wagonjwa wa
selimundu ili kunusuru maisha yao kutokana na kwamba, Tanzania inashika nafasi
ya nne duniani kwa kuwa na wagonjwa wengi wenye selimundu.
Baada
ya wazazi hao kuongea na waandishi wa habari leo, MNH na Wizara ya Afya imetoa
ufafanuzi juu ya usitishwaji huduma hiyo ambapo imewataka wagonjwa kufuata
utaratibu wa uhamisho ili wakapate huduma katika hospitali zilizopo karibu yao.
MNH
kupitia Museru imesema kuwa, wagonjwa waliokuwa wanatibiwa hospitalini hapo
kurudi kwenye hospitali za mikoa na kwa wale ambao wako katika hatari
wanaruhusiwa kutubiwa Muhimbili baada ya kupata barua za rufaa.
“Muhimbili
huduma bado ipo, haijasitishwa kama inavyosemwa na baadhi ya watu,
iliyositishwa ni huduma ya bure, wagonjwa watakaopata rufaa ya kutibiwa
hapa watachangia huduma kama ilivyo kwa wagonjwa wengine,” amesema.
Magembe
amesema, wagonjwa walidhani kuwa huduma hiyo inatolewa na Muhimbili pekee na
kuwa, hospitali zilizokaribu nao kuna kliniki za wagonjwa waselimundu.
Dorothy
Gwajima, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Tiba Wizara ya Afya amesema, tangu awali
huduma za wagonjwa wa waselimundu zilikuwa zinalipiwa na kuongeza kuwa, kama
kutakuwa na mgonjwa asiyekuwa na uwezo anaruhusiwa kuomba msaada kupitia dawati
la utawi wa jamii.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni