Zinazobamba

MASIKINI MBUNGE MTEMVU WA JIMBO LA TEMEKE,AZOMEWA JUKWAANI MPAKA AKIMBIA,NI MATOKEO YA NGUVU YA UMMA,SOMA HAPO KUJUA


Pichani wakati kati ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Temeke,Abbas Mtevu,
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Temeke kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM,Abbas mtemvu imemlazikia kushuka kwenye jukwaa alilokuwa akilitumia kunadi sera,baada ya umati mkubwa wa vijana kumzomea pamoja na kumrushia chupa za maji.Anaadika KAROLI VINSENT endelea nayo.
    Tukio hilo la aina yake limetokea Leo Majira ya asubuhi kwenye viwanja vya mwembe Yanga wakati Mgombea huyo alipokuwa anawatubia Vijana wa “joking” kutoka maeneo mbali mbali ya  Temeke jijini Dar es Salaa wakati alikuwa akiwaomba wamchagua tena kuwa Mbunge katika Jimbo hilo.
      Mtemvu licha ya mkutano wake huo kusindikizwa na wasanii wanaotamba kwa miziki ya uswahilini inayojulikana kama  “vigodoro” wasanii hao ni  Dogo Diga pamoja na Dj Man fongo ambao wote kwa pamoja walikuwa ni wa kwanza kupanda katika jukwaa wakiimba huku wakishangiliwa na vijana mbali mbali waliokuwepo Uwanjani hapo,
       Mara baada ya kumaliza kuimba wasanii hao wa "visingeli",ndipo ikafika wakati wa Mtevu kupanda Jukwaani na kuwaeleza nia ya yeye kutaka kuendelea kugombani Ubunge kwa awamu nyingine ya Nne katika jimbo,
      Ndipo aliposhika kipaza sauti akianza kujinadi, huku akisema “CCM oyee” jambo liliwachukiza watu waliokuwepo uwanjani hapo, ndipo nao wakaanza kutoa ishara inayotumiwa na mgombea Urais kupitia Chadema ,Edward lowassa ambaye anaungwa mkono na Vyama vya Ukawa, yakuzungurusha mikono huku wakiimba kwa pamoja “Lowassa mabadiliko,mabadiliko Lowassa”huku wakimzomea Mbunge huyo,
        Jambo lilomfanya Mtevu kushindwa hata kuzungumza na ikamlazimua kushuka jukwaani hapo na kuondoka Uwanjani hapo kuebuka Vurugu,
   WANANCHI WA TEMEKE WA NENA.
Wakizungumza kwa wakati mmoja  na fullhabari.blog,wananchi wa jimbo la Temeke waliokuwa uwanjani hapo wamesema,Hawamtaki mgombea huyo wa CCM kwani katika kipindi cha miaka 15 alichokuwa mbunge hakuna alichokifanya kwenye jImbo hilo.
     “Huyu bwana amekaa zadi ya mika 15 hakuna alichofanya amekuwa Mbunge wa kulala Bungeni huku akishindwa hata kutusaidia sisi wakazi wa Jimboni kwake,tumemchoka bora aondoke kabisa na leo hii ni trela muvi kamili ataiyona octoba 25 hatuitaki CCM tena”Amesema ally Said mkazi wa Temeke.
 Mbali na huyo Mkazi, mwengineni Mama Juma naye pia alimtupia lawama Mbunge huyo kwa kusema miaka yote aliyokuwa Mbunge wa Jimbo la Dar es Salaam,ameshindwa kuoka wizi unaofanywa na Mameya wa jiji.

“Yaani amekuwa mbunge,miongoni mwa majimbo ya Dar es Salaam,amehusika kwa maksudi katika kunyamazia uuzwaji wa bei ya kutupwa,shirika la usafirishaji wa Uda,kwa familiya ya vigogo wa Ikulu,leo anakuja kutulilia sisi,kwa taarifa yake ndio hajue kwamba hatumtaki”amesema mama huyo.

Hakuna maoni