Zinazobamba

ACT WAZALEONDO YAONYWA SOMA HAPO KUJUA


Karatu. Baadhi ya wakazi Jimbo la Karatu, mkoani Arusha wameonyesha kukerwa na kitendo cha mgombea mwenza wa Chama cha ACT-Wazalendo, Hamad Yusuf cha kumponda mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa.
Wamekitaka chama hicho kunadi sera zake badala ya kumzungumzia mtu kinapoendelea na kampeni zake jimboni humo, la sivyo watasusia mikutano yao ya kampeni.
Akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika juzi katika Viwanja vya Mazingira Bora, mgombea huyo wa ACT - Wazalendo, alidai kuwa Lowassa amekwenda Chadema siyo kwa kutaka urais, bali kutafuta kusafishwa kutokana na kashfa ya ufisadi.
Alipomaliza kutoa kauli hiyo, baadhi ya watu waliokuwa wakimsikiliza walianza kuondoka uwanjani hapo wakidai kuwa amewakera kwa kauli yake hiyo.
Mkazi wa Karatu Stendi, Simon Jackson alisema mgombea huyo asiwavuruge, hawakuja kusikiliza tuhuma na matusi katika mkutano huo bali sera.
“ACT-Wazalendo isituvuruge, hatuwezi kumkataa Lowassa kwa sababu eti alikuwa fisadi, mbona hawajamshtaki mpaka sasa, atuambie chama chake kitatufanyia nini,” alisema Jackson.
Alisema mgombea mwenza huyo anapaswa kujenga hoja za kuwashawishi wananchi.
Naye Mariam Olesaiki, alisema Karatu wanahitaji kiongozi atakayewaletea mabadiliko ya kuwa na serikali ya majimbo aliyodai itawapatia fursa ya kufaidika na rasilimali zao moja kwa moja.
“Nchi yetu ina vyanzo vingi vya mapato, tunachotaka kusikia katika mikutano ya kampeni ni fedha za Ngorongoro zinachangia kiasi gani kwenye bajeti ya Taifa siyo fulani kafanya nini,” alisema Philemon Urio.
Akizungumza katika mkutano huo, mgombea urais wa ACT - Wazalendo, Anna Mghwira alisema wakati umefika wa kuiondoa CCM madarakani.
Alisema kazi hiyo itashindikana kama wananchi hawatataka kubadilika na kuendelea kuipa kura CCM.
“Liwake jua inyeshe mvua, lazima tuiondoe CCM madarakani,” alisema na kuongeza:
“Huu ni mwaka wa mabadiliko na ni wa wanawake, tunahitaji rais mwanamke au sio baba zangu na mama zangu,” aliuliza mgombea huyo na kujibiwa “ndiyo”.


Hakuna maoni