LOWASSA AMCHANGANYA JANUARY MAKAMBA,SASA ALIA NA MAGAZETI KUHUSU LOWASSA,SOMA HAPO KUJUA
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJj1oqPP9GoSd_SB-CFYp8JqLY-ajpZ3gYMAZpzBp1ftcl1SJLPmE9jf6yIpGEB9gNMaUOKztEtgCr9P3bemh8AuGYFLhAVA5yvIF07nB75WeB3C82EtC4coXT0vTheVUkLc_3_meQZqA/s1600/1.jpg)
NA KAROLI VINSENT
WAKATI chama
cha Mapinduzi CCM kikituhumiwa kuyatumia Magazeti ya Uhuru,Tazama,Dira Mtanzania,Mikakati
pamoja na Raia Tanzania kuripoti habari za kiplopaganda na za kizushi kwa
Mgombea wa Urais kupitia Chadema Edward Lowassa,
Sasa CCM ni kama kimeanza kuweweseka na kusema
Magazeti nchini yanampendelea Lowassa,
Hayo
yamesemwa na Mjumbe wa Kamati ya Kampeni ya CCM, January
Makamba ameonesha kutokubaliana kwake na ripoti za kinachojili kwenye mikutano
ya mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa na kueleza kuwa Magazeti
hutumiwa kupiga kampeni.
Makamba ameeleza hayo kupitia mtandao wa Twitter baada ya mtu
mmoja anaetumia jina la ‘Gachanja Muigai’, kumueleza kuwa kutokana na kile
wananachokisoma, inaonekana kuwa wananchi wengi wanamuunga mkono Lowassa. Na
akataka kupata maoni ya Makamba kutokana na hali hiyo kama anadhani wataweza
kushinda.
“@JMakamba @MagufuliJP From what we read here, it seems #Lowassa is resonating with Wananchi. Una hakika si wakati wa kuvuka sakafu?” Aliuliza.
Makamba alimjibu kuwa wapinzani wanatumia baadhi ya magazeti kama sehemu ya kampeni zao lakini tafiti na hali halisi nchini inaeleza tofauti.
“They’ve turned some newspapers into their campaign fliers. But the polls & mood across Tanzania tell another story.”
Mpekuzi blog
Maoni 1
januari makamba kwa maana nyingine anatangaza uhasama wa kujitakia baina ya waandishi wengi wa habari ndani na nje ya nchi na chama chake-ccm- anawashambulia kwa sababu tuu hawairembi na kuipendelea ccm.kazi ya uandishi ni kazi ya dhamana na heshima kubwa kwa jamii.siku zote jamii inawategemea waandishi wawahabarishe,habari za kweli na si vinginevyo.waandishi wanasafiri,wanahoji,wanasikia na,wanapaswa-kwa haki na ukweli-kuanndika uhalisia wa matukio,na,ndivyo wanavyofanya.kwa hali hiyo januari na chama-dola ccm wananchi wako upande wa lowasa na wajue kwa sasa wajiandae tuu mnamo novemba kukaa upande wa pili wa bunge letu kama chama kipya cha upinzani.muda wao umewadia,hakuna jinsi.
Chapisha Maoni