Zinazobamba

RAIS KIKWETE AWACHIA KILIO WABUNGE WA CCM,NI KUHUSU AHADI ZAKE ZA 2010,SOMA HAPO KUJUA

Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala

AHADI zilizotolea na Rais Jakaya Kikwete wakati wa kuwania urais mwaka 2010, zimeonekana kuwatesa wabunge wengi wa CCM kutokana na nyingi kutokamilika na hivyo kuwaweka njia panda katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Anaandika Dany Tibason … (endelea). 
         Hali hiyo ilijitokeza bungeni leo wakati wa kipindi cha maswali na majibu, ambapo wabunge wengi waliihoji serikali ni lini ahadi hizo zitakamilika.
      Mbunge wa Magu, Dk. Festus Limbu (CCM) katika swali la nyongeza alitaka kujua ni lini serikali itatekeleza mradi wa maji katika mji wa Magu.
       Naye Mbunge wa Kahama, James Lembeli (CCM) akauliza ni lini serikali itatimiza ahadi mbalimbali za ukamilishaji wa miradi ya maji katika jimbo hilo.
       “Kuna ahadi nyingi ambazo zilitolewa na Rais Kikwete lakini cha kushangaza miradi hiyo haijatekelezwa sasa ni lini serikali itaweza kukamilisha ahadi hizo.
          “Naitaka serikali itoe kauli ni lini itaweza kutekeleza ahadi hizo ili wananchi waondokane na adha ya maji ambayo inawafanya kushindwa kufanya shughuli nyingine za kimaendeleo? Amehoji Lembeli.
         Awali katika swali la msingi la mbunge wa Magu, alitaka kujua ni lini serikali itatekeleza ahadi ya kuwapatia maji ya uhakika wananchi wa mji wa Magu na ahadi hiyo imefikia wapi.
        Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Maji, Amoss Makala, amesema ahadi zote zilizotolewa na Rais zitatekelezwa.
        Hata hivyo, amesema tatizo kubwa ambalo linasababisha miradi kutokutekelezeka kwa wakati ni kutokana na ufinyu wa bajeti.
        Amesema serikali imekuwa ikijitahidi kuhakikisha miradi mbalimbali ya maendeleo inatekelezeka japo changamoto kubwa ni ukosefu wa fedha ya kutosha.
Kwa hisani ya mwanahalisi oline


Hakuna maoni