Zinazobamba

WAHISANI SASA WAKUBALI KUACHIA FEDHA,- NI BAADA YA KURIDHISHWA NA SAKATA LA ESCROW

 
Waziri wa Fedha saada  Mkuya akifafanua jambo kuhusu wadau wa maendeleo kukubali kutoa fedha walizoahidi kuipatia serikali ya Tanzania kama msadaa na kisha kuamua kusitisha baada ya sakata la Escrow, Mkuya amesema wahisani wamekubali kutoa fedha hizo, Wahisani wanaosaidia bajeti ya Tanzania ni pamoja na African Development Bank (AfDB), Canada, Denmark, Umoja wa Ulaya, Finland, Germany, Ireland, Japan, Norway, Sweden, Uingereza na Benki ya Dunia.

Wadau wakimsikiliza waziri wa fedha pindi alipokuwa akifafanua jambo kuhusu wahisani kuachia fedha kwa serikali ya Tanzania.

Kufuatia hatua ambazo serikali zimeshughulikia sakata la Escow, sasa wadau wa maendeleo na benki ya Dunia wamewkubali kwa kauli moja kuachea fedha kwa serikali ya Tanzania katika bajeti ijayo ili serikali iweze kupanga mipango yake vizuri,
Akizungumza na waandishi wa habari mapema hii leo, Waziri wa Fedha , Mh. Saada Mkuya amekili kuwa sasa wahisani wamekubali kuachia fedha ,ili serikali ipange mipango yake ya kimaendeleo pasipo kikwazo kutoka kwa wahisani,
Mkuya amesema hatua ya wahisani kukubali kutoa fedha hiyo inatokana na wahisani hao kuridhishwa na hatua ambazo serikali imezichukua katika kushughulikia sakata la Escrow ambalo limekuwa sababu ya wao kusitisha misaada kwa serikali,
Mkuya ameendelea kusema kuwa Kwa jinsi ambazo wamekubaliana Wahisani hao wataanza kuachia jumla ya Dola 44 Milion kwanza  na baadaye wataziachia fedha nyingine ambazo kimsingi walikubaliana kuzitoa katika serikali ya Tanzania,
Nao banki ya Dunia imeahidi kutoa fedha Takribani Dola Milion 227 kwa serikali ya Ttanazania hapo baadae ili kusapoti bajeti ijayo
 Ilikuwa ni  Alhamisi, Novemba 6, 2014, Waziri mkuu hakusita kuonyesha masikitiko yake na ya nchi yetu kwa ujumla kwa kitendo cha wahisani kuzuia misaada ya Jumuiya ya Ulaya zikiwamo pia Norway, Canada, Japan, Benki ya Dunia na hata Benki ya Maendeleo ya Afrika.
Wahisani hao walisitisha kutoa fedha kwenye Bajeti Kuu, kiasi cha dola za Marekani 558 sawa na shilingi bilioni 937 ambazo sasa baada ya kuridhishwa wameamua kuachia fedha hizo kwa serikali yetu
Kulikuwa na maneno mengi sana yalisemwa juu ya wahisani kusitisha fedha hizo,wengine walifika mbali na kusema kwamba wahisani hao  wanaamua bila kufanya mazungumzo ya kina na wanaowahisani. Laiti wahisani wangekaa chini na Serikali kuzungumzia azma yao ya kusitisha misaada yao kwa bajeti kuu, naamini, kuwa wangepata ufahamu mkubwa juu ya mchakato wa sakata hilo ulivyo, na kwamba wangevuta subira kusubiri matokeo ya mchakato huo. Sasa mambo yamekaa sawa, fedha zitatoka tu kama walivyokubaliana.


Wafadhili wa mataifa ya nje kwa Tanzania walisimamisha misaada yao kwa serikali ya Tanzania wenye thamani ya karibu Dola za kimarekani Milioni 558 sawa na Pauni za kiingereza Milioni 311 ambazo zingetumika katika kusaidia bajaeti ya Taifa.
Hatua hiyo ilikuja kufuatia madai ya ufujaji wa pesa unao walenga baadhi ya maofisa wa juu wa serikali ya Tanzania wanaotuhumiwa kuchota kiasi cha pesa kutoka katika Benki kuu kwa kivuli cha mikataba ya Nishati.
Mbunge wa Kigoma Mh. Zitto Kabwe ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya PAC ndiye alipigilia msumari wa sakata hilo baada ya kusema kuwa maofisa kadhaa wa ngazi za juu serikalini walishirikiana na wafanya biashara wabadhirifu kuhamisha kiasi cha Dola Milioni 122 kutoka katika Benki Kuu ya Tanzania kwenda katika akaunti ya Benki binafsi.
Wahisani wanaosaidia bajeti ya Tanzania ni pamoja na African Development Bank (AfDB), Canada, Denmark, Umoja wa Ulaya, Finland, Germany, Ireland, Japan, Norway, Sweden, Uingereza na Benki ya Dunia.
Antila aliongeza kuwa "Serikali ya Uingereza haina uvumilivu kwa rushwa na udanganyifu, na kwa kushirikiana na wahisani wengine, haitofadhili bajeti nyingine yeyote kwa Serikali ya Tanzania mpaka tutakapoona madai haya yanashughulikiwa na serikali ipasavyo".
Benki ya Dunia na wahisani wengine kwa muda sasa wamekuwa wakisaidia katika miradi mingi ya ujenzi yenye thamani ya zaidi ya dola za kimarekani milioni 230.

Hakuna maoni