Zinazobamba

SERIKALI YA KIKWETE YASHIKWA PABAYA NA CHAMA CHA ADC CHAIBUKA NA WASEMA YA KWAO SOMA HAPA

Pichani ni Mwenyekiti  wa Cha cha (ADC)   Said Miraaj Abdulla
Akizungumza na waandishi wa Habari mda huu
Jijini Dar es Salaam

CHAMA cha kisiasa cha Alliance for Democratic Change(ADC)kimeitaka serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuwageukia watanzania waliokata tama na maisha kwa mfumo wanaodai ni wakinyonyaji.
      Aidha,Chama hicho pia kimesikitika  kusuasua kwa serikali katika kutatua matatizo  yanayowakumba Watanzania ikiwemo majanga mbalimbali ambayo yametokea hivi karibuni ikiwemo mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi wa Albino.Anaandika KAROLI VINSENT Endelea nayo
          Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa chama cha ADC Taifa,Said Miraaj Abdulla wakati wa mkutano na waandishi wa habari ili kuzungumzia hali ya masha kwa  Watanznaia ambapo amesema  hivi sasa nchini kuna matukio mengi ya vifo vinavyoweza kuzuilika ambavyo anadai katika hali ya kawaida hakuna anaelalamika kuomba vifo hivyo vikomeshwe.
           “Kiukweli  kunapotokea matatizo makubwa ikiwemo hili la mvua ya mkoani kahama tumeshuhudia  viongozi mbalimbali wengine hudiriki hata kutoa rambirambi za mamilioni kwa wafiwa ili waonekane kwenye luninga,hali ya kuwa marehemu hawajawai kumuona,na huku mtoaji huyo huyo mrehemu hawajawai kumuona”amesema Abdulla.

Waandishi wa Habari wakiwa kazini 

        Abdulla ameongezeka kuwa wananchi wamekuwa wakikumbana na matatizo mengi lukuki ikiwemo tatizo la umasikini,ajira,na tatizo la ombwe la uongozi huku serikali bado ikiwa hajawaweka njia ya kutatizo.
        Alaibainisha kuwa kwa kusema  hadi lini wanyonge wataendelea kufa huku akidai wakubwa wakifaidi matunda ya kutibiwa nje wao na familia zao tena kwa gharama za kodi inayolipwa na masikini wanao kufa kwa maradhi mbalimbali.
             Katika hatua nyingine chama chicho cha upinzani nchini kimesikitika kwa kile wanachesema ni dharau kwa serikali iliyopo madarakani kwa kitendo chake cha kushindwa kuwachukulia hatua watendaji mbalimbali waliopelekea hadi kutokea kwa ajali mbaya gari iliyotokea juzi mkoani Iringa na kupolekea vifo vya watu zaidi ya 48.
‘Hii ni serikali gani isiyokuwa na uchungu kwa wananchi ni serikali gani isiyoshtuka na vifo vya watu zaidi ya 48,huko iringa leo tumemsikia mkuu wa mkoa huo akisema basi lilobeba abiria lemezidisha watu,hivi jamani hebu tujiulizeni ilo basi limepita maeneo mbalimbali huku polisi wabarabarani wakiliangalia tu,kama hii ingekuwa serikali makini –“
         “Ingechunguza pindi  basi hilo linapita maeneo yote mpaka linapata ajali na lingechunguza nani alikuwepo barabarani  na nani alikuwa kwenye vituo vya uchunguzi na wangechukuliwa hatua maana hapa kuna mambo ya Rushwa “amesema Abdulla.
             Vilevile,Abdulla amelitupia Lawama jeshi la Polisi nchini kwa kitendo chake cha kuwafedhehesha wananchi ambao wanatuhumiwa na matukio mbalimbali ya uharifu kuwaonyesha kwenye luninga kuwa ni watuhumiwa bila ya kuwa na ushahidi huku watuhumiwa hao wakipelekwa mahakamani wanashinda kesi na jeshi la polisi halirudi kwasafisha kama limewakuta hawana makosa.

     Bwana Abdalla ametoa wito kwa watanzania kutovumilia  hujuma zinazofanywa na serikali badala yake amesema ni wakati wa kuacha kulalamika ni mda wakufanya maamuzi magumu kuindoa serikali iliyoko madarakani.




Hakuna maoni