Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO-MAASKOFU WAISUSA CCM,NI KUHUSU MAHAKAMA KADHI,WASEMA LIWALO NA LIWE,SOMA HAPA KUJUA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete

JUKWAA la Wakristo nchini limetaka waamini wake, kutopigia kura Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani, unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu. Anaandika Saed Kubenea…(endelea).
         Uamuzi wa kutaka waamini wa madhehebu ya Kikristo wasichague CCM, umefikiwa katika mkutano wa jukwaa hilo uliofanyika katika ukumbi wa Baraza la Maaskofu, Kurasini jijini Dar es Salaam, Jumanne wiki hii.
     Mtoa taarifa wa amekiambia chanzo changu kuwa maaskofu walifikia uamuzi huo baada ya kuchoshwa na walichoita, “kigeugeu cha serikali katika kushughulikia Katiba Mpya na Mahakama ya Kadhi.”
             Mkutano wa Maaskofu ulijadili kwa kina suala la Katiba Pendekezwa na Mahakama ya Kadhi, pamoja na masuala mengine, ikiwamo usalama wa nchi ulivyo kwa sasa na mustakabali wake.
         Mwamvuli wa Jukwaa la Wakristo Tanzania, ni jumuiko la pamoja la Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT).
          Vyanzo vya taarifa kutoka ndani ya mkutano vinamnukuu Askofu mmoja mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kulutheli Tanzania (KKKT) akisema, kanisa limetuhumu serikali kushindwa kuchukua hatua kutokomeza vitendo vya kigaidi, mauaji ya albino na uvunjifu wa amani.
Aidha, kanisa limetuhumu serikali kutaka kuingiza nchi katika vita vya kidini kwa kitendo chake cha kutaka kuruhusu kuwapo kwa Mahakama ya Kadhi na mahakama hiyo, kutambulika na sheria za nchi.
       “Katika hili la Mahakama ya Kadhi na Katiba Pendekezwa, maaskofu walikuwa wakali sana. Kwa kweli, wametoa matamshi ambayo hayajawahi kutolewa na viongozi wa kidini, tangu kanisa kuumbwa nchini,” ameeleza kiongozi mmoja wa kidini aliyehudhuria mkutano huo.
          Amesema, “Maaskofu wamekasirishwa na kitendo cha Mizengo Pinda (waziri mkuu), kubeba suala la Mahakama ya Kadhi, kama suala lake binafsi ili kutimiza adhima yake ya kutaka kuwa Rais.”
           Akizungumzia Katika Pendekezwa, mtoa taarifa anasema, maaskofu hawataki kura ya maoni ipigwe kwa kuwa wamejiridhisha mchakato wa Katiba, umeligawa taifa na serikali imeshindwa kusimamia zoezi la kura ya maoni.
         Amesema, “katika kutilia mkazo hoja hiyo, jukwaa la Wakristo likasisitiza waumini wake kutokipigia kura CCM.”
Katika tamko lake, Jukwaa limesema, “…kwa kuwa chama tawala na serikali yake wameshindwa kusimamia misingi iliyolea taifa kama serikali isiyo ya kidini na taifa lenye amani; umoja na utulivu; linawaelekeza waumini wote na wenye mapenzi mema, wakati wa uchaguzi mkuu ujao kufanya maamuzi yanayolitanguliza taifa badala ya kutanguliza mazoea, mapokeo, itikadi na ushabiki wa chama fulani cha siasa.”
Chanzo cha Mwanahalisi.online


Hakuna maoni