Zinazobamba

HIVI NDIVYO NIT WALIVYO WAKARIBISHA FIRST YEAR, HAKUNA ALIYKAA KWENYE VITI, YABAINIKA HAIJAWI KUTOKEAAA...

Kama kawa furaha mwanzo mwishooo, hakuna kulala,haya ndio mambo ya wana NIT, fullbata mwanzo mwisho

ILIKUWA  ni nderemo vifijo katika ukumbi wa hadhi za kimataifa wa  Jangwani uliopo maeneo ya kawe, ambapo wanafunzi wa chuo cha Taifa cha ushafirishaji walipokuwa wakijiachia katika shoo kabambe ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka mpya katika chuo hcho ambacho kwa sasa kinaonekana kuchukua wanafunzi wengi sana
Katika shoo hiyo wanafunzi walipata fursa mbalmbali ya kucheza kunywa, pamoja na mashindano ya kuogelea ambayo awali yalielezwa na uongozi kungekuwa na zawadi lakini mpaka tunaenda mitamboni hakuna alilipwa kwa ajiri ya kuoga,
  
VIWANJWA VYA CHUO
Majira ya kama saa kumi na moja hivi wanafunzi hao walionekana kuwa na mishe mbalimbali katika viwanja vya chuo, hali ilionyesha wazi kuwa siku hiyo mambo yatakuwa ya  hali ya juu katika ukumbi wa Jangwani ambao ama hakika fullhabari ilipofika hapo iligundua kuwa na utofauti mkubwa na kumbi ambazo wanafunzi wa chuo hicho mara nyingi walikuwa wanafanyia sho zao za kuwakarisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza,

Kwanza nikiri wazi kuwa kutokana na usafiri ambao fullhabari iliutumia kufika eneo la tukio, ilikuwa imechelewa kwa kiasi kikubwa matukio muhimu ambayo Eng Zakaria Mganilwa aliwanasibu wanafunzi hao wapya wanayoanza makazi mapya katika chuo hicho cha usafirishaji, lakini hiyo haizuii kukupa taarifa muhimu ambazo zilijiri baada ya mkuu huo ambaye amepania kuleta mapinduzi makubwa ndani ya chuo chake kumaliaza hutuma yake,

Fullhabari ilifika rasmi katika viwanjwa vya Jangwani majira ya saa tano usiku ambapo tayari mkuu huyo ameshafanya majumusho yake kwa wanafunzi hao, kilichoendelea hapo ni hiki hapaa!!!!!!
Ndo kama hivi mazeee, mdada huyu alikutwa akiwa anacheza kiduku cha aina yake huku wakiwa katika mvua kubwa ya ARTIFICIAL

Hii ndo habari ya mjini baana, miongoni mwa wanafunzi wa chuo cha taifa cha usafirishaji akipozi kwa picha,
Si nia yangu kueelezea kuwa debe lilirukwaje, maswali hayo yatajibiwa na picha ambazo utaziona punde, hapa lengo langu kubwa ni kutaka kuufahamisha ummma wa Serkali ya wanafunzi wa Sonit kuwa fulsa nzuri zinapotkea ni wakati wa kuzitumia ipasavyo na kinyume chake fursa kama hizo zinaweza kukomesha na hivyo  kuwanyima fursa vizazi vijavyo kufurahia maisha japo kwa siku moja,

MATUKIO YA AJABU AMBAYO NI VEMA SESERA UKAJIPANGA 
Mwanadada mmoja anayesadikiwa kuwa anasoma kozi ya logistics na usafirishaji ngazi ya cheti, mkondo A (picha tunazo za ugomvi)inadaiwa aling'ara vilivyo baada ya kufanikisha kuwasababishia mashabarobaro walikuwa wanammendea mendea kuzichapa kavukavu wakidai mdada huo wote ni wakwao, 

Hakika nilishangaa kama, wakati kama huu bado kuna wadau tena ambao wanaheshimika katika chuo hicho wakawa na katabia ka shule za msingi, nilipojaribu kudadadisi ikabainika kuwa wote hao ni wanafunzi wa mwaka wa kwanza, hivyo walikuwa wanajaribu bahati kwa mwanadada huyo anayekimbiza mbaya katika darasa hio la BCLTM A




viduku navy vilikuwapo, hapa mmoja wa wadau wa chuo hicho wakifurahi katika siku hiyo ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza

kama kawa kawa hii ndiyo tabia ya wanafunzi wa chuo cha taifa cha usafirishaji, sijui hapa anamaana gani ,mimi na wewe hatujui, kama huyu anatarajiwa kuwa afisa wa uchukuzi una coment gani hapo wazee




No comments