Auawa kwa kukutwa uchi mgodini
MKAZI wa Kijiji cha Kapanda, wilayani Mlele, Katavi, Yunge Maboja (70), amefariki dunia baada ya kushambuliwa na wananchi kwa kupigwa na silaha za jadi, ngumi na mateke baada ya kukutwa akiwa uchi kwenye shimo la kuchimba dhahabu.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahili Kidavashari, alisema
Maboja alishambuliwa juzi, saa 7 usiku katika Kijiji cha Kapanda
wakimtuhumu alikuwa akiroga ili mwenye shimo hilo asipate dhahabu.
Alisema wiki tatu kabla ya tukio hilo, Maboja alimuazimisha Idd
Kipara shoka alilokuwa akitumia katika shughuli zake, alipokuwa
akimtafuta mtu aliyemuazimisha alichungulia ndani ya shimo ambalo
walikuwemo watu wawili wakichimba madini.
Kamanda Kidavashari alisema watu hao walishitushwa na kitendo cha
kuchunguliwa muda huo, hivyo iliwalazimu marehemu akiwa mtupu.
Alisema ndipo watu hao; Abui na Hassan walipoanza kumshambulia kwa
maneno ya kashfa kuwa ni mchawi na ndiyo maana amefika kwenye shimo lao
akiwa uchi, hali inayochangia wasipate madini kwa muda mrefu.
Kidavashari alieleza kuwa walimshambulia kwa fimbo na mateke na
kumlazimisha awapeleke kwa mwenyeji wake, Juma Ngegeshi ili awapatie
uchawi, lakini walimkuta mkewe, Asha Shabani ambaye alieleza hakuna
kitu wanachohitaji, hali iliyochangia naye kuanza kushambuliwa kwa
fimbo usoni na mgongoni.
“Asha alipiga mayowe ya kuomba msaada na ndipo majirani walipofika na
kumkuta Maboja akiwa uchi, nao waliungana kuwashambulia.
Kidavashari alieleza majeruhi wote wawili walifikishwa kituo cha
polisi cha Mpanda na baadaye kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda
ambako Maboja alifariki dunia akiwa anaendelea kupatiwa matibabu.
Jitihada za kuwasaka wahusika wa tukio zilifanyika na polisi
inawashikilia watu wawili ambao ni Yunge Hassan (43) na Ayub
Samwel (30) kwa mahojiano.
Wakati huo huo, Raia wa China, Chen Gungson anayemiliki kampuni ya
uchimbaji madini ya Got Accident on Ming Camp, amefariki dunia baada ya
kutumbukia ndani ya shimo la mgodi wa dhahabu katika machimbo ya Ibidi,
wilayani Mlele.
Tukio hilo lilitokea juzi, saa 3 asubuhi wakati raia huyo wa China
alipokuwa akikagua maeneo anayofanyia shughuli za uchimbaji dhahabu.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya wilaya.
No comments
Post a Comment