Zinazobamba

JUKWAA LA KATIBA KUONGOZA TAASISI ZISIZO ZA KISERIKALI KATIKA KUPATA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA, WENYEWE WASEMA WATAPELEKA WAJUMBE 20 KWA MH. RAIS KIKWETE

Na mwandi wetu,,
Daresalaam

Kaimu Mwenyekiti wa jukwaa la katiba Bw. Hebron Mwakagenda akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari mapema hii leo jijini daresalaam,Mwakagenda  amesema Jukwaa hilo la katiba limeamua kuchukua jukumu la kuongoza taasisi zisizo za kiserikali katika kuteua wajumbe wa kuwakilisha katika bunge la katiba

Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makinitaarifa ya kaimu mwenyekiti juu ya kuwaongoza taaasisi zisizo za kiserikari NGOS, kuteua wajumbe 20 katika bunge la katiba.

Tunafuatilia, waandishi wa habari wakiwa makini na kazi yao wakifuatilia maelezo ya kaimu mwenyekiti, katika mkutano huo, jukwaa la katba limebainisha wazi vipengele vitakavotumika kupata wajumbe wa kuwakilisha katika bunge la katiba

Mjumbe akifafanua kwa hisia, wajumbe kama hao kutoka taasisi mbalimbali hapa nchini watakutana mjini dodoma kujadili ni nani aweze kuingia katika bunge la katiba. jumla ya wajumbe 20 wanatarajiwa kupishwa siku hiyo toka taasisi mbalimbali


MMOJA WA WAJUMBE AMBAO WALIHUDHULIA KATIKA MKUTANO HUO WA WAANDISHI WA HABARI AKIFAFANUA JAMBO KWA HISIA, MJUMBE HUYO AMESEMA, SUALA LA BUNGE LA KATIBA LINAHITAJI UMAKINI WA HALI YA JUU SANA, NA WAJUMBE WATAKAO WAKILISHA WANANCHI KATIKA BUNGE HILO LA KATIBA NI VEMA WAKAWA MAKINI,
katibu wa jukwaa la katiba akisikiliza hoja za waandishi wa habari waliokuwa wanataka kufahamu ni vigezo gani vinatumika kuwapata wajumbe hao 20 toka katika taasisi zisizo za kiserikali zaidi ya 1000?. Katibu amesema vigezo vitakavyotumika ni pamoja na uwakili wa Kijiografia na uwakilishi wa Kisekta

SIKU chache baada ya Rais  Jakaya Kikwete kuitisha makundi kupeleka mapendekezo ya majina ili aweze kuteua wajumbe wa Bunge la Katiba.Nalo Jukwaa la Katiba nchini limechukua hatua ya kuongoza Taasisi zisizo za kiserikali katika kuteua wajumbe hao.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo kwenye ofisi za Makao makuu ya Jukwaa la Katiba nchini jijini Dar es Salaam Kaimu Mwenyekiti wa jukwaa hilo Hebron Mwakagenda amesema Jukwaa hilo la katiba limeamua kuchukua jukumu la kuongoza taasisi zisizo za kiserikali katika hatua hii.

“Jukwaa la katiba limechukua hatua ya kuongoza Taasisi zisizo za za kiserikali na pia tumeandaa mkutano mkubwa utakaofanyika New Dodoma Hoter tarehe  30 mwezi huu, tunataradadi  mkutano huu utakaoudhuriwa na wajumbe wapatao 200 toka kila mkoa na wilaya za Tanzania Bara na Zanzibar”alisema Mwakagenda.

Vilevile Mwakagenda aliongeza na kusema dhumuni la mkutano huu  ni kuchagua wajumbe  wanaopenda kuingia kwenye Bunge la katiba.
“Mkutano huu tutakua na kazi ya kuchagua wajumbe wanaopendekezawa kuingia kwenye  Bunge la katiba ili kumwezesha Rais kuteua wajumbe 20 miongoni mwao kwa mujibu wa sheria ya Mabadiriko ya katiba sura ya 83 ya mwaka 2013”


“Mara baada ya zoezi la uchaguzi wa wajumbe tutamwandikia barua Rais kumsihi aweze kuteua wajumbe 9 kutoka kwenye uwakilishi wa kijiografia na wajumbe  na wajumbe 11 kutoka kwenye uwakilishi wa kisekta ili kuwa na uwakilishi mpana”alifafanua Mwakagenda.

Katika hatua nyingine  Jukwaa hilo la Katiba hapa nchini limewataka makundi mengine yaliyotajwa kwenye sheria,kuitisha mikutano ya kidemokrasia kuchagua wajumbe wao na kuyapeleka kwa Rais kikwete  ili aweze kufanya uteuzi  wa mwisho.

Tamko hili la Jukwaa la katiba limekuja baada taarifa iliyotolewa na Ikuru ikonyesha mwisho wa kupeleka majina ni tarehe 2 mwezi ujao.Na makundi hayo yaliyobainishwa kwenye sheria ni,Taasisi zisizokuwa za Kiserikali,Taasisi za kidini,vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu,Taasisi za Elimu ya Juu, Makundi yenye ulemavu,Vyama vya wafanyakazi,Vyama vya wafugaji,Vyama vya wakulima na vyama vinavyowashirikisha wavuvi. 

VIGEZO VYA KUWAPATA WAJUMBE 20 TOKA TAASISI MBALIMBALI ZISIZO ZA KISERIKALI

Akizungumzia namna ya kuwapata wajumbe wajumbe 20 toka taasisi mbalimbali, Mwakagenda amesema tayari wameamua kuitisha mkutano mkubwa wa taasisi zisizo za kiserikali mjini dodoma kujadili suala hilo, 
Wajumbe watapatikana kwa vigezo vya uwakilishi wa kiigeografia, katika kipengele hiki kutakuwa na uwakilishi wa kanda ya ziwa, ambako kuna mikoa ya Kagera Mwanza, Geita,Simiyu na Mara,

Kanda ya kati kutakuwa na mikoa ya Singida,Dodoma,na Morogoro, wakati kanda ya Magaharibi kutakuwa na mikoa ya Shinyanga Tabora,Katavi, na Kigoma
Kanda nyingine ni kanda ya Pwani itakayokuwa na mikoa ya Daresalaam na Pwani yenyewe, 

Kanda ya kaskazini kutakuwa na mikoa ya Kilimanjaro,Arusha,Manyara,na Tanga, Kanda ya nyanda za juu kusini Kutakuwa na mikoa ya Iringa Njombe, Mbeya na Rukwa, kanda ya kusini kutakuwa na mikoa ya Ruvuma,Mtwara, na Lindi

Kanda zingine ni Kanda ya Unguja amboyo ina mikoa yote ya unguja  na kanda ya mwisho ni kanda ya pemba yenye mikoa yote ya Pemba.


 

No comments