Zinazobamba

RAIS NYUSI WA MSUMBIJI KUFANYA ZIARA YA SIKU NNE TANZANIA



Na Mussa Augustine.

Rais wa Msumbiji Philip Jacinto Nyusi anatarfajwa kuwasili Nchini Tanzania  kwa ziara yake ya kikazi ya siku nne kuanzia Julai 1 hadi 4 ,2024 ikiwa ni muendelezo wa  mahusiano ya nchi hizo mbili yaliyodumu kwa muda mrefu.

Taarifa hiyo imetolewa  leo Juni 30,2024, jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh.Januari Makamba wakati akizungumza na waandishi wa habari nakubainisha kuwa Rais Nyusi anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania kufuatia mwaliko maalumu wa  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.

Waziri Makamba amesema kuwa Rais Nyusi ndie anaetarajiwa kuwa mgeni rasmi atakayefungua maonyesho ya 48 ya biashara ya kimataifa (Saba saba) Julai 3, 2024 baada ya hapo ataelekea Zanzibari.

 “Ukiangalia kuna raia wa Msumbiji wapo Tanzania wakifanya shughuli zao za kiuchumi ,na sisi Watanzania  wapo Msumbiji wakifanya shughuli za kiuchumi  hivyo siyo jambo la kushangaza kuendelea kudmisha  ushirikiano na uhusiano wetu ambao umekuwa wa muda mrefu sasa”amesema Waziri Makamba.

Nakuongeza kuwa “Ziara hiyo itaanzia pale Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere Julai 1 ,atapokelewa na Viongozi wa mbalimbali na tarehe 2 atakutana na Rais Samia Suluhu Hassan ikulu, ambapo watafanya mazungumzo ya faragha watajadili mambo mengi ikiwemo ushirikiano wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili ili kuimarisha mahusiano yetu.

Aidha Waziri Makamba pia amesema  katika ziara hiyo mikataba kadhaa itasainiwa ambapo itahusu ushirikiano katika Sekta Mbalimbali ikiwemo Sekta ya Afya, Elimu , Madini pamoja na Habari lengo ni kuongeza mahusiano mazuri hususani katika kuimarisha ulinzi na usalama baina ya nchi hizo mbili hususani maeneo ya mpakani


Hata hivyo amesema kuwa biashara kati ya nchi hizo mbili bado sio nzuri kutokana na biashara ambazo zinafanyika  mpakani hazirekodiwi ambapo Tanzania ndio imekua ikipeleka bidhaa nyingi zaidi Msumbiji kuliko nchi hiyo kuingiza Tanzania

No comments