Serikali na wadau wa Elimu watakiwa kuwekeza nguvu katika elimu ya Kidijitali ili watoto waendane na Dunia ya leo
Umoja wa Mameneja na Wamiliki wa shule na vyuo visivyo vya serikali (TAMONGSCO) Umeiomba serikali Pamoja na wataalamu mbalimbali wa elimu kushirikiana, ili kuwawezesha Watoto kuweza kuyatumia vizuri mabadiliko ya kudijital kwa kuyageuza mabadiliko hayo kuwa uwanja mzuri wa kujifunzia na kupanua uwanja wa watoto kujisomea ili kusiwepo na mtoto anayeachwa nyuma.
Hayo yameelezwa mapema Mei 8, 2022 na Alfred Luvanda ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Mameneja na Wamiliki
wa Shule na Vyuo visivyo vya Serikali (TAMONGSCO) wakati akiendesha mashindano
ya Chemsha Bongo baina ya shule 10 za jijini Dar es salaam.
Aidha Mwenyekiti
huyo amesema kuwa hii ni kama sehemu ya kuendeleza utamaduni wa kujisomea na
kujiendeleza katika elimu kuwa uwepo wa Majukwaa ya Kidijital yenye kutoa fursa
kwa Watoto kuweza kujisomea masomo mbalimbali shuleni kwa njia ya dijital ikiwemo
Jukwaa la TESEA.
Ameongeza
kuwa ni hatua muhimu ya kuweza kuungana na wengine kuwasilisha suluhu
zinazounganishwa na Teknolojia ili kusiwe na mtoto atakaye achwa nyuma, kwa kuhakikisha
kila mwanafunzi anapata nyenzo za kujifunzia kupitia majukwaa ya kidijitali sanjari
na mataifa mengine duniani ili kufanya taifa kunufaika na maendeleo hayo ya
Teknolojia.
![]() |
| Baadhi ya wanafunzi waliyoshiriki katika mashindano hayo ya Chemsha Bongo. |
Aidha kwa
upande wa Mkurugenzi wa Dijital Academia Limited (DATL) Mombo Kaleo amesema
muda wa sasa kwenye elimu ni kwenye Dijitali kwani hiyo ni njia pekee inayoweza
kumuhakikishia kila mwanafunzi wa kitanzania kupata nyenzo zote za kujifunzia
kwenye ncha za mikono yake.
Ameendelea kusema
kuwa si nyenzo tu bali ni nyenzo zilizo sawa na mtaala wa taifa na kuwafanya Watoto
kuwa na matumizi mazuri ya mabadiliko ya Dijitali.
![]() |
| Shughuli ikiendelea. |



No comments
Post a Comment