Zinazobamba

Redcross(TRCD),imetoa msaada wa fedha kwa kaya 500 katika wilala ya Mburu na Simanjiro

Na Yasmine Protace

TANZANIA Redcross(TRCD),imetoa msaada wa fedha kwa kaya 500 katika wilala ya Mburu na Simanjiro,ambapo Wilaya hizo zimeathiliwa na ukame.
Msaada huo ulikabidhiwa na Katibu mkuu wa Tanzania Redcross Sociéy , Felician Mtahengerwa ambaye aliambatana na mwenyekiti wa Redcross wakili  Moses Basila. .

Katika kugawa msaada huo pia mkurugenzi wa Maendeleo ya Taasisi na Miradi Reginald Mhango ameungana na wafanyakazi wa TRCS na IFRC katika zoezi la kugawa msaada wa kifedha kwa kaya 500.

"Kaya zilizo athirika na ukame ni  200 katika  wilayani simanjiro,Mkaoni Manyara ,"alisema.

Aliongeza kuwa   kaya  hizo 200  zimenufaika na msaada huo wa TRCS chini ya ufadhili wa IFRC.
Katika  msaada huo, Katibu wa RedCross amekutana na mkuu wa wilya ya simanjiro Suleiman Serera ambaye ameipongeza Red Cross kwa kazi zake nakusema anawakaribisha muda wowote kwa ushirikiano

Serera ameiomba   TRCS kuangalia uwezekano wakusaidia Wilaya hiyo  program za kutokomeza ukame .

Kwa mujibu wa Katibu wa TRCD zoezi la kugawa msaada zoezi lilianza Aprili 27 mwaka huu  wilayani Mburu amabapo kaya 100 zilinufaika  na hivyo kuleta jumla ya kaya 300 mkoani humo.

Kwa mujibu wa Katibu huyo pia kaya 200 za Mburu Mkoani Arusha zilinufaika na zoezi  hilo.


No comments