Zinazobamba

Mwamko sekta ya Islamic Banking wazidi kuimarika, NBC warudi kwa kishindo

 


Meneja mahusiano wa Benki ya maendeleo ya NBC Tanzania Bw Ally Abdul amewaomba Waislam na wasio waislam kuipokea benki hiyo kwa mikono miwili kwenye huduma ya Islamic Banking kwani sasa wameamua kurudi kwa nguvu kubwa kuhudumia jamii ambayo kiasili hawapendi kutumia benki ambazo zinatoza riba.

Akizungumza na Waislam Mei 6, 2022 kwenye swala ya Ijumaa iliyofanyika katika msikiti wa Mtambani Jiji Dar es Salaam, Abdul alisema benki imedhamiria kutoa huduma bora kwenye sekta hiyo.

“NBC ndio waanzilishi wa huduma za kifedha kwa mfumo wa Kiislam Tanzania, ilianza Mei 5, 2010, lakini kutokana na sababu zisizo zuilika ikawa haikuwa kwenye matangazo mengi, ndio maana ikawa kama iko chini, ispokuwa kwa sasa NBC tumerudi, tena tumerudi kwa nguvu kubwa, tutatumia mifumo yetu ambayo imeenea kila sehemu Tanzania kutangaza Islamic Banking,” alisema

Aidha, Mtaalam huo wa masuala ya mahusiano ya umma alisema benki yao imejipanga vizuri kuhakikisha huduma wanazotoa zinafuata sheria zote zinazoongoza sekta hiyo na tayari wanayo bodi yenye weledi mkubwa wa kushughulika na masuala hayo.

Pia alisema kwa sasa benki ya NBC wanabidhaa aina mbili, mosi ni akaunti za akiba lakini bidhaa ya pili ni biashara ya mikopo.

“Kwenye upande wa kuwekeza tunayo La riba saving akaunti, la Riba business akaunti na Privilege akaunti kwa ajili ya watu wanaohitaji huduma yenye upekee hasa wafanya biashara,

Vilevile, ipo akaunt ya La riba Fixed Akaunti, ambayo upekee wake mkubwa ni kwamba inayo uwezo wa kuenda mpaka miaka 5, “Yaani mteja anaweza kuwa na fedha yake mfano laki 5 au million 5, 10, 100 basi anaweza kuja kuiweka benki kwa muda anaotaka, ikumbukwe wakati fedha yake ikiwa benki itafanyiwa biashara na atapata gawio,” alisema

Aidha, akifafanua gawio linavyopatikana, Abdul alisema fedha inayowekwa katika akaunti ya Fixed inakopeshwa kwa wateja kwa kufuata misingi ya uislam na faida inayopatikana inagawanya pande mbili, benki na mmiliki wa fedha.

“Namna ya kuchukua gawio husubil mpaka miaka mitano iishe, faida yake inaweza kuchukua muda wowote, kuanzia miezi mitatu, miezi sita, mwaka na kadharika,”alisema

La Riba Busines akaunti ni kwa ajili ya wafanyabishara, unakuta mtu ana fedha nyingi hataki zikae nyumbani, anataka kuweka benki ili achukue kwa kuendesha biashara yake.

Mbali na biashara hiyo ya kuwekeza fedha benki, pia NBC inafanya biashara ya mikopo isiyo na riba maarufu kama murabaha.

“Tunatoa mikopo kwa ajili ya wafanyakazi chini ya uaratibu wa murabaha, lakini pia tunatoa mikopo ya biashara pamoja, katika biashara hii haihusishi fedha kabisa, tunafanya hivi ili kuepuka riba,” alisisitiza Bw. Abdul

BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) ni moja ya benki kubwa hapa nchini ambayo inatoa huduma zinazo sifiwa.


No comments