Zinazobamba

Mkurugenzi Kituo cha Kimisri aaga Waislam Mtoro, aacha wosia mkubwa





Ni miaka mitatu sasa toka Mudiri wa Markaz Chang’ombe Sheikh Abdul-Mu’ty afike nchini kuendeleza mafundisho sahihi ya uislam kwa Taifa la Tanzania. Hivi


sasa kiongozi huyo anayetibu nyoyo muda wake wa kuishi nchini umekwisha na anatarajia kurejea nchini kwake Misri hapo Mei 8, 2022. Gazeti imaani limebahatika kufanya mahojianao naye likitaka kujua baadhi ya mambo kadhaa, ungana na Suleiman Magali kuelewa kwa kina zawadi aliyowaachia watanzania

 

Mwandishi wetu: Wewe kiongozi mkubwa wa Markazi hii na unaondoka mei 8, 2022 baada ya kukamilika muda wako, pengine upi ushauli wako kwa waislam wa Tanzania

 

Sheikh Abdul-Mu’ty: Yapo mengi ya kushauri lakini kubwa nililoliona ni umuhimu wa Mufti wa Tanzania katika kuenenza dawa, huyu ni mtu safi sana, niwaombe Viongozi wa Tanzania, Maimamu na Masheikh wajitahidi kumuunga mkono, wajitahidini sana kuwa nyuma yake kwani ni kiongozi aliyebalikiwa tabia nzuri ukarimu na usamehevu.

 

Mwandishi wetu: Msomaji angependa kujua mambo ambayo hutayasahahu hata ukiwa nchini Misri katika kipindi chako chote ulichoishi hapa nchini

 

Sheikh Abdul-Mu’ty: Nikili kuwa sitasahahu ushirikiano mzuri ambao nimepewa na ofisi ya Bakwata nchini Tanzania na Taasisi zingine. Waislam wa Tanzania ni watu wakarimu sana na wanao penda dini.

 

Kipekee nikili kuwa sijawahi kuona kiongozi mwenye sifa nzuri kama za Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zubeir, kiongozi huyu ni msamehevu, mpenda watu, mpole, mkirimu, anawajali wayonge mafakiri, na masikini. Nimeishi nchini Misri na kukutana na viongozi Mbalimbali, lakini mfano wa Mufti Zubeir bado sijapata kuona.

 

Lakini jambo la pili ambalo sitasahahu hata nikiwa wapi ni mashindano ya quran. Sijawahi kuona sehemu yeyote mashindano ya quran yanafanyika kwenye uwanja mkubwa kama wa Mkapa na watu wakafurika vile. Hili jambo limeacha alama katika nafsi yangu. Sijawahi kuona sehemu yeyote duniani watu wenye mahaba na quran kama Tanzania.

 

Mwandishi wetu: Kitu gani una jivunia katika kipidi chako cha uongozi katika kituo hiki cha Kimisri

 

Sheikh Abdul-Mu’ty: Yapo Mengi ya kueleza, lakini kiufupi mimi kwa kushirikiana na wenzangu tumeweza kuendesha semina mbalimbali za kuelezea kwa kina fikra sahihi ya uislam. Tumeendesha semina hizo ndani ya kituo lakini pia nje ya kituo. Hapa niwashukuru sana Bakwata wamekuwa wakitoa ushirikiano mkubwa kufanikisha shughuli za kidaawa. Hakika naondoka lakini moyo wangu bado upo Tanzania. Ni sehemu sahihi ya kufanya kazi kwani watu wake ni wakarimu na wenye upendo wa hali ya juu.

 

Mwandishi wetu: Jambo gani limekufurahisha hapa Tanzania?

Sheikh Abdul-Mu’ty: Tanzania ni nchi ya amani na upendo, nimependa watu namna wanavyopendana, kuthaminiana na kujaliana bila kujali dini, rangi.

 

Licha ya kuwa na dini tofauti lakini siku zote watanzania wamekuwa wamoja, hilo ni jambo kubwa na ni nadra kuliona katika mataifa mengine.

 

Kituo cha Markazi Chang’ombe shabaha yake ni kudumisha amani, nimefurahi zaidi baada ya kuona watanzania wamekuwa mstali wa mbele kudumisha amani.

 

Uislam ni amani na sisi shabaha yetu ni kuufundisha uislamu wa kweli, kuonyesha sura sahihi ya uislamu, kuna watu waliuchafua sana uislamu na watu wanadhani huo ndio uislamu

 

Mwandishi wetu: Jambo gani linakukera na ungetamani litafutiwe ufumbuzi mapema?

 

Sheikh Abdul-Mu’ty: Jambo ambalo bado linanisikitisha ni kutokukubalika kwa vyeti vya chuo cha Azhar Sharif hapa Tanzania. Sisi hapa chuoni tunaona jambo hili haliko sawa, kwa sababu tunaona watoto wetu ni kama wanabaguliwa, masomo yanayosomwa yangeweza kuwa msaada katika taifa, tunatoa vijana wazuri waliolelewa kimaadili, wenye kukataa dhulma.

 

Unakuta mtoto anatumia muda mwingi kusoma, akimaliza masomo yake hapati kazi serikalini, sababu zakukosa kazi sisi bado hatuelewi.

 

Vile vile idadi ndogo ya wanafunzi nayo ni jambo ambalo linatushughulisha, chuo kwa miaka yote imekuwa inatoa huduma zake bure, inafundisha vijana bila kuwatoza kitu chochote, lakini Chuo kimeenda mbali Zaidi, sasa hivi kimeongeza idadi ya wanafunzi wanaokwenda kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo, zamani kilikuwa kinapeleka wanafunzi 4, lakini baada ya maombi mbalimbali chuo kimekubali kuongeza idadi ya watanzania kwenda kusoma kutoka wanafunzi 4 hadi kufikia 30, Licha ya uwepo wa nafasi hizo, bado vijana wameendelea kupungua katika Markazi zetu.

 

Historia ya Kituo cha kimisri Tanzania…

 

Kituo cha Markaz Chang’ombe kilianza mwaka 1965, kilipatikana kama zawadi iliyotokana na mahusiano mazuri baina ya serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania iliyokuwa inaongozwa na Rais wa kwanza wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na baba wa Taifa hili, Hayati Mwl Jurius  Kambarage Nyerere, na Serikali ya Misri.

 

Kwa pamoja walikubaliana kuja na kitu hiki, kituo kilizinduliwa rasmi  na kufanya kazi zake mwaka 1968, kilizinduliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mwl. Jurius Nyerere.

 

Kituo kimeendelea kuwa kitovu cha mahusiano mema baina ya serikali hizi mbili toka miaka hiyo hadi hivi sasa.

 

Kupitia kituo cha Kimsri vijana wengi wa kitanzania wamepata elimu na kujikomboa katika maisha yao, lakini kimekuwa tanuru la kuzalisha walimu wazuri wa dini ambao wanafundisha uislamu sahihi hapa Tanzania. Vijana wengi wa Kimisri wamepata fursa ya kuja nchini kufundisha dini,

 

 

 

Mafanikio Makubwa ambayo yamepatikana toka kuanzishwa kwake ni pamoja na uwepo wa mahusiano mema kati ya kituo na Serikali, kupitia kituo hiki na mahusiano mazuri yaliyopo Kampuni za nchini Misri zimefanikiwa kupata tenda ya kujenga Mwalimu Nyerere electric Project ambayo zamani ilikuwa ikifahamika kama stiglesr George.

 

Mbali na mahusiano ya kidiplomasia pia kwenye upande wa dini, chuo kimepata mafanikio makubwa ikiwemo kuweza kufundisha wanafunzi wengi Tanzania bara na visiwani.

 

Takribani mikoa na wilaya zote za Tanzania zina wanafunzi kutoka Markazi, pia katika taasisi nyingi za kidini viongozi wake wakubwa ni mazao kutoka chuo cha Azhar Shariff. Vilevile kwenye nyumba za ibada nyingi wanaoongoza swala ni wanafunzi kutoka kituo cha kimisri. Kwa ujumla Kituo cha Kimisri kimekuwa ni muhimili mkubwa wa kueneza elimu ya dini hapa nchini.

 

Mazao ya kituo hiki ni pamoja na Sheikh Suleyman Muhammad Gorogosi, huyu baada ya kurejea kutoka Misri alifanikiwa kushika nafasi kubwa katika Baraza kuu la waislamu Tanzania (BAKWATA), alifanikiwa kuwa Naibu Mufti wa Tanzania.

 

Mwingine ni Sheikh Ali Muhidini Mkoyogole, yeye amefanikiwa kuwa Naibu Chifu Kadhi Mkuu wa Tanzania.

 

Wamo pia Sheikh Ali Ngeruko, ambaye ni mjumbe wa Baraza la ulamaa taifa, Sheikh Shabani Musaa ambaye ni Katiku Mkuu wa Baraza la Sunna Tanzania (BASUTA), Waziri Amani Maduga wa mkoani Morogoro.

 

Wengine ni Sheikh Twahir Khaidary Mwinyimvua imaan wa  msikiti wa Mwinyikheri, Sheikh Abdallah Nyumba, Imaam wa msikiti wa Qibratain uliopo Kariakoo, Tanzania na Sheikh Alhad Musa, ambaye ni Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

 

Masheikh wa Wilaya wapo Sheikh Zairai Bakari Mkoyogole ambaye ni Sheikh wa Wilaya ya Temeke, Sheikh Adam Mwinyipingu ambaye anahudumia Wialaya ya Ilala na Sheikh Mohammad Ahmadi Mulenga anayefanya kazi katika Wilaya ya Kinondoni.

 

 

 

No comments