Zinazobamba

TIC yapokea Wawekezaji Kutoka Qatar ambao Wamekuja kuangalia Fursa za Uwekezaji


Wawekezaji kutoka Qatar wakiwa katika mkutano wa majadiliano katika ofisi za Tic jijini Dar es salaam.

Na Mussa Augustine.

 Kituo Cha Uwekezaji Nchini (TIC) kimepokea wawekezaji wapatao 25 kutoka Nchini Qatar ambao wamekuja kuangalia fursa za Uwekezaji katika sekta mbalimbali hapa Nchini.

 Akizungumza na wanahabari Mara baada ya kupokea wawekezaji hao Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bi. Anna Lyimo  amesema ujio wa wawekezaji hao unatokana na ziara iliyofanywa hivi karibuni na Viongozi wa TIC  ambao walienda nchini Qatar nakufanya mazungumzo na baadhi ya Wafanyabiashara kutoka shirikisho la Wafanyabiashara la Qatar KERALA BUSINESS FORUM.

 " Ujio wa wageni hawa unatokana na mwendelezo wa kuhamasish na kuwavutia wawekezaji,hivyo wawekezaji wapatao 25 wamekuja kuangalia fursa ya kuwekeza Kati sekta mbalimbali ikiwemo Mifugo,Vifaa tiba,Utalii,Madawa, sekta ya anga pamoja na masuala ya uchumi wa Bluu" amesema Anna.

 Aidha amesema Kwamba kutokana na kuwepo kwa diplomasia nzuri ya Uwekezaji pamoja na kufungua milango kwa wawekezaji hao wawekezaji wengi wa kigeni wameanza kujitokeza huku akiwasihi wawekezaji wa ndani wajiunge na TIC waweze kupata taarifa mbalimbali za fursa ya Uwekezaji Nchini.

 Amendelea kusema kuwa wawekezaji hao wanatarajiwa Machi 29 kutembelea Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuangalia fursa ya Uwekezaji lakini kwa Sasa TIC inawapitisha katika taratibu mbalimbali za Uwekezaji pamoja na masuala ya vibali vya kuwekeza Nchini.

Kwa upande wake Raisi wa Shirikisho la wafanyabiashara Nchini Qatar Bw.Shanavas Bava amesema kwamba wamekuja kuangalia fursa zakuwekeza hapa Nchini kutokana na Tanzania kuwa na fursa nyingi lakini pia kuwepo na mazingira mazuri yakiuwekezaji ni jambo lililowavutia kuja kuwekeza.

 Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Lanchi ya Taifa( NARCO) Bw. Petter Msofe amesema mazao mengi ya Mifugo Kama vile nyama ya Mbuzi,Ng'ombe na Kondoo yamekuwa yakitumika sana Mjini Doha Nchini  Qatar hivyo wawekezaji hao watasaidia kikuza sekta ya Mifugo nakuongeza pato la Taifa.

 " Hivi karibuni tulihudhulia mkutano mkubwa wa Kilimo na Mazingira uliyofanyika mjini Doha Nchini Qatar,tulishirikiana na ofisi ya balozi wa Tanzania Nchini Qatar,Doha wanapenda sana kula nyama inayotoka kwetu hivyo wawekezaji wameanza kuja kuwekeza, na sisi tunaendelea kuunga Mkono serikali ya rais Samia Suluhu Hassan ambaye ameonyesha nia ya kufungua milango ya uwekezaji"amesema Be.Msofe.

 

No comments