KC KIVULE YAADHIMISHA SIKU YA MWANAMKE DUNIANI KWA KUTOA ELIMU YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WANAFUNZI WA ABUUY JUMAA SEKONDARI.
Katika kuendelea kuhenzi siku ya Mwanamke duniani ambayo uhadhimishwa kila mwaka ifikapo Machi 8, Kituo cha Taarifa na Maarifa kata ya Kivule kimekutana na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Abuuy Jumaa iliyopo ndani ya kata hiyo na kuwapa elimu ya masuala ya kijinsia.
![]() |
| Picha ikionyesha kongamano la maadhimisho ya siku ya wanawake katika shule ya Sekondari Abuuy Jumaa. |
Akiongea na mtandao
wa full Habari Mwenyekiti wa Kituo hicho Bi. Zahara Omary Mzee amesema kuwa lengo
la kituo hicho kuamua kuadhimisha siku hiyo Pamoja na wanafunzi hao, ni kuweza
kuwashirikisha mambo mbalimbali yanayohusu Afya, Uchumi Pamoja na elimu ya Ukatili
wa kijinsia.
Aidha ameongeza
kuwa wanafunzi Zaidi ya 300 wamepata elimu hiyo ambapo kwa upande wa uchumi
wameweza kuwafunza jinsi ya kufanya kilimo cha mjini, ambapo mboga uoteshwa
kwenye viroba, lakini pia wameweza kuwafundisha namna ya kugeuza taka taka kuwa
nishati mbadala ya kupikia na kuokoa gharama za kununua mkaa.
Ameendelea kusema
kuwa katika elimu ya ukatili wa kijinsia wamewapa wanafunzi hao mbinu
mbalimbali za kukabiliana na ukatili huo, lakini pia njia za kuzuia ukatili
usitokee au kutoa taarifa endapo watakabiliwa na vitendo vya aina hiyo.
Na mwisho amelipongeza
shirika la TGNP kwa kuweza kuwawezesha kwa kuwapa elimu mbalimbali za ukatili
wa kijinsia Pamoja na ujasiriamali ambazo wao kama kituo wamekuwa wakizisambaza
kwa watu na makundi mengine ndani ya jamii.
Kwa upande
wake Mratibu wa chanjo kutoka hospitali ya Wilaya ya Kivule Dr. Helfrid Mpolo
amesema kuwa wamewapa wanafunzi elimu juu ya saratani ya kizazi Pamoja na tezi
dume ili wafahamu namna ya kujilinda na kuepuka visababishi vya maradhi hayo.
Ameongeza kuwa
kundi lililopo hatarini Zaidi kupata maradhi haya ya Saratani ya Shingo ya
mlango wa kizazi ni umri kuanzia miaka 14 na kuendelea na kuwataka Watoto hao
kuweza kuacha ngono zembe kwani ni moja ya kisababishi kikubwa cha ugonjwa huu.
Na mwisho ameendelea
kuwataka wazazi na walezi kuacha tabia za kuwakataza Watoto kuchoma Chanjo ya Saratani
ya shingo ya mlango kizazi kwa kufananisha chanjo hii na ile ya Uviko 19, na
kuwahakikishia kuwa chanjo hii haina madhara yotote na ni salama kwa Watoto wao.
Kwa upande
wake Mkuu wa shule hiyo ya Abuuy Jumaa Bi. Floida K. Nkya amesema kuwa wao kama
uongozi wa shule wamefurahishwa sana na elimu hiyo iliyotolewa shuleni hapo, kwani itawasaidia Watoto wao kuweza kujitambua
na kupambana na changamoto mbalimbali za kiafya na ukatili wa kijinsia ndani ya
jamii.
Ameendelea kutoa
wito kwa wadau na Taasisi zingine kuweza kuiga mfano wa Kituo cha Taarifa na Maarifa
Kivule kwa kuweza kushiriki siku ya Wanawake Duniani na Watoto wa shule hiyo
ikienda sambamba na elimu nzuri ya kujitambua, na kuendelea kukitaka kituo
hicho kiwe na programu za mara kwa mara katika shule hiyo.








No comments
Post a Comment