Zinazobamba

PAUL KIMITI :AZUNGUMZIA MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 100 YA BABA WA TAIFA JULIUS KAMBARAGE NYERERE




Mwenyekiti wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Paul Kimiti (pichani juu) akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya maadhimisho ya miaka mia moja ya kuzaliwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yanayotarajiwa kufanyika  april 13 mwaka huu.

 Na Mussa Augustine

Taasisi ya Kumbukumbu  ya Mwalimu Nyerere inatarajia kufanya makongamano yakumuenzi baba wa Taifa hayati Julius Kambarage Nyerere ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha kumbumkumbu ya Miaka 100  tangu Kuzaliwa kwake mwaka 1922.

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Mheshimiwa Paul Kimiti amesema kwamba ifikapo Aprili 13 baba wa Taifa atakua anatimiza miaka100 tangu Kuzaliwa, hivyo makongamano hayo yatafanyika kikanda yakienda sambamba nakufanya shughuli za kumuenzi baba wa Taifa katika mikoa yenye historia zake,pamoja na kuendeleza agenda yakitaifa ya  Upandaji wa miti.

Aidha Kimiti amesema kwamba Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere enzi za uhai wake alisimamia falsafa ya kulinda amani ,kuondoa ubaguzi, nakuwafanya Watanzania waweze kuishi kwa upendo,mshikamano pamoja  na kujitegemea,ambapo falsafa hizo zinapaswa kuenziwa kupitia Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu  nyere ili kuwafanya  vijana na jamii kwa ujumla kuzifahamu.

Aidha Mwekiti huyo ameongeza kwamba jamii inapaswa kuendelea kuzijua kazi alizozifanya baba wa Taifa katika kulikomboa Taifa nakwamba kuenzi juhudi hizo kutalifanya Taifa kuendelea kulinda misingi ya amani,mshikamano na upendo nakuondoa ubaguzi miongoni mwa jamii ya kitanzania.

" Mwalimu Nyerere angekua hai  April 13 angetimiza Miaka mia moja  tangu Kuzaliwa kwake,tumeamua kufanya kumbukumbu ya Kuzaliwa kwake kwa kufanya makongamano ambayo yatafanyika kikanda natutafanya shughuli Mbalimbali za kumuenzi kikanda,tutanzia kanda ya Ziwa pale Butiama alipozaliwa,kanda ya kaskazini,kanda ya kati (Dodoma) ,Kanda ya kusini na Kanda ya Magharibi,na kumalizia Dar es salaam na Zanzibar” amesema Kimiti.

Nakusisitiza kwamba" kila Kanda kutafanyika  shughuli katika mikoa yenye historia za Mwalimu Nyerere  na  Taifa kwa ujumla, pamoja na kufanya zoezi la Upandaji miti, kutakua na makongamano yatakayozungumzia falsafa za mwalimu kulingana na historia ya mikoa iliyopo kwenye Kanda hizi jinsi ilivyohusika katika kuendeleza kudumisha amani,upendo na mshikamano.

Kwa upande wake  Katibu Mkuu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere  Simon Lubugu amesema kwamba viongozi waliopo kwa Sasa ni wale waliozaliwa Miaka ya hivi karibuni hivyo hawajui misingi ya baba wa Taifa ilivyokua ,hivyo kupitia Taasisi hiyo watapata fulsa yakujua misingi ya baba wa Taifa aliyowajengea Watanzania enzi ya uhai wake.

" Viongozi wengi wa Sasa wamezaliwa Miaka ya themanini hivyo wamekua sio wazalendo kwa Taifa kwansababu hawajui misingi iliyoachwa na muasisi wa Taifa hili,kuanzishwa kwa Taasisi hii itasaidia Sana vijana hawa waliozaliwa kipindi hiki na kijacho kufahamu misingi hiyo iliyoachwa na Baba wa Taifa." Amesema Lubugu.



Mjumbe wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu DOKII wakwanza kutoka mkono wa kulia akiwa na Mhamasishaji wa Taasisi hiyo Mtiti Mbassa Jirabi aliyepo katikati wakisikiliza ujambo kutoka kwa Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Paul Kimiti hayupo pichani wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es salaam

 Mjumbe wa Taasisi hiyo Ummy Wenceslaus alimaarufu kwa jina la “DOKII” amewasisitiza vijana kuona umuhimu wakujiunga na Taasisi hiyo kutokana na mchango wa baba wa katika kulijenga Taifa la Tanzania pamoja na mataifa mengine hasa katika kujenga misingi ya amani,mshikamano na upendo pamoja na kuzisaidia baadhi ya nchi za barani afrika kupata uhuru.

Halikadharika amewataka wasanii kutumia sanaa zao kupaza sauti juu yakumuaenzi baba wa Taifa katika jamii ili kuendeleza mazuri ambayo ameacha  kama alama ya upendo kwa Taifa,huku akiwaasa pia viongozi walioko madarakani kuyaishi kwa vitendo yale yote aliyoanzisha baba wa Taifa.

"Ni vyema viongozi wa sasa waziishi falsafa za baba wa Taifa kwa vitendo kwani falsafa zake zimesaidia  kuleta ukombozi kwa Taifa na mataifa mengine Barani Afrika."Amesisitiza Dokii.

Mkutano huo na waandishi wa habari umefanyika katika ofisi za taasisi hiyo zilizopo Makonde Beach Dar es salaam na umeudhuliwa pia na mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa Taasisi hiyo Balozi Mstaafu Francis Mndolwa, pamoja na mhamasishaji wa taasisi hiyo Mtiti Mbassa Jirabi ambao kwa nyakati tofauti wameelezea umuhimu wa kumuenzi baba wa Taifa hayati Julius Kambarage Nyerere.
 

No comments