NDC YAWATAKA WANAWAKE WACHANGAMKIE FURSA YA UWEKEZAJI WA VIWANDA
Na Mussa Augustine
Ikiwa leo ni kelele cha Maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani serikali kupitia Shirika la Maendeleo Nchini (NDC) imesema itahakikisha inaboresha mazingira ya uwekezaji wa Viwanda ili kuwafanya wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wavutiwe kuwekeza miradi mbalimbali itakayo chochea ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa Ujumla.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika ilo Nicholaus Shombe wakati
akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es salaamu wakati akielezea
mikakati iliyojiwekea NDC katika
kuhakikisha inawanufaisha wawekezaji katika masuala ya Uwekezaji wa Viwanda.
Dr.Shombe
amewaomba Watanzania waendelee kuliamini Shirika lao la Maendeleo la Taifa(NDC)
kwasababu lina miradi mikubwa ambayo inatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa ya
viwanda nakwamba tayari kuna baadhi ya wawekezaji kutoka mataifa yakigeni yameonyesha
nia yakuwekeza katika viwanda vya kuunganisha magari.
Mkurugenzi
huyo Mtendaji amesema Kwamba NDC kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (
TANESCO) wameanza kutatua kero ya kukatika kwa umeme Mara kwa Mara,pamoja
nakuimarisha mfumo wa upatikanaji wa maji ya uhakika ili kuwafanya wawekezaji
wawe na mazingira bora ya Uwekezaji.
Afisa Uhusiano wa NDC Mirian Chavalla wa kwanza kushoto akitoa maelezo ya miradi mbalimbali inayotekeleza na shirika hilo mbele ya Mkurugenzi Mtendaji Dr. Nicholaus Shombe wakati alipotembelea banda la shirika hilo Katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jiji Dar es salaam
"Tuna miradi mingi mikubwa ambayo tunaitekeleza,kuna Mradi wa Magadi Soda Mradi huu nimkubwa sana,ukizungumzia Makemoko ya Viwanda unazungumzia Magadi soda ,hivyo nawaomba Watanzania waendelee kuliamini Shirika lao la Maendeleo, namimi nikiwa kama mkurugenzi mtendaji kwa kushirikiana na timu yangu tutahakikisha tunaleta mabadiliko makumbwa ndani ya shirika " amesema Dr.Shombe.
Nakuongeza
kwamba "Tunataka tuwe na NDC yatofauti, shirika lipo kwa ajili
yakuwasaidia watanzania,na maadhimisho haya ya siku ya mwanamke Duniani tupo
hapa kuwambia wanawake kwamba NDC ipo kwa ajili yao ,wachangamkie firsa ya
uwekezaji wa viwanda.
Aidha amewataka
wanawake kuelekea maadhimisho yasiku ya mwanamke Dunia inayoazimishwa Machi 8
kila mwaka ,wajitokeze kuchangamkia fursa ya uwekezaji wa viwanda vya nguo
kwenye kongani ya Viwanda ya NDC iliyopo kibaha Mkoani Pwani ili kuwafanya
wanawake wazawa wanufaike na Viwanda.
Dr.Shombe
ambaye ametembelea maonyesho ya bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na wanawake
kupitia viwanda vidogo ambayo yanafanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini
Dar es salaam,ambapo amefurahishwa na kazi kubwa wanayoifanya.
No comments
Post a Comment