SERIKALI YATOA MAELEKEZO SITA KWA WAWEKEZAJI WA SEKTA YA MADINI
Na Mussa Augustine
Serikali imeagiza mambo sita kwa wawekezaji wa katika sekta ya Madini Nchini ikiwemo kuzingatia uhifadhi wa Mazigira na kutokujihusisha na utoaji wa ajira kwa Watoto Migoni.
Maagizo hayo
yametolewa na Makamu wa Raisi Dr.Philip Mpango wakati akifungua mkutano wa siku
mbili wa Kimataifa wa uwekezaji katika sekta ya Madini Tanzania 2022.
Mkutano huo ambao una
kaulimbiu “Mazingira wezeshi kwa Maendeleo ya sekta ya Madini Tanzania”umewakutanisha
wadau wa uwekezaji katika sekta hiyo kutoka ndani na nje ya Nchi.
Dr. Mpango ametaja
mambo mengine kuwa wawekezaji wenye ubia na serikali waharakishe utekelezaji
kwa mujibu wa makubaliano ili wananchi
waanze kunufaika.
“Suala la uharibifu
wa Mazingira nina wakumbusha wachimbaji wote wakubwa na wadogokuzingatia sheria
za mazingira ,wawekezaji wote mnawajibu wa wakuhakikisha shughuli zenu za
uchimbaji,uchenjuaji,uchakataji wa madini zinatekeleza kwa mujibu wa
sheria na taratibu” amesema Dr.Mpango
Aidha Makamu huyo wa
rais pia amewataka wawekezaji wote hususani wakubwa wazingatie matakwa
yatokanayo na tathmini ya athari kwa mazingira na jamii kwa kuzingatia misingi
ya uzalishaji endelevu ,matumizi na mbinu bora za uzalishaji wa teknolojia bora
na rafiki kwa Mazingira.
Ambapo jambo lingine
amezikumbusha kampuni zote za uwekezaji katika sekta ya Madini zihakikishe
zinatekeleza ipasavyo Matakwa ya kisherika ya kuandaa mipango ya ufungaji
migodi na kuweka hati fungani ya urekebishaji wa mazingira.
Hata hivyo amezitaka Benk na taasisi zingine za fedha kushirikiana na shirika la Madini (STAMICO) kubuni namna bora zaidi ya kuwaqwezesha wachimbaji wadogo wakati serikali ikiendelea kuzifanyia kazi suala la kuanzishwa kwa benki maalumu ya madini.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Madini Jonh Bina ametaja baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni pamoja na mitaji ambapo taasisis za fedha hutoa mikopo kwa wawekezaji wa uchimbaji dhahabu nakuwaacha kuwasaidia wendine.Nae Waziri wa Mdini
Dotto Biteko amesema uwekezaji mkubwa unaondelea kwenye utafiti wa Madini maeneo mbalimbali ni uthibitisho tosha wa
dhamira ya serikali ya kuwekeza katika sekta hiyo muhimu.
No comments
Post a Comment