Zinazobamba

Brela yawaita wana-Dar es salaam Mliman city, wapiga kambi siku tano

Afisa Habari wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Sheila Mfunami akifafanua jambo kwa mteja, Bw. Frank Mmbali katika maonyesho ya Brela yanayoendelea Viwanja vya Mlimani City. Brela imepiga kambi ya siku tano kuanzia leo January 26-30, 2022


Afisa Tehama wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Joram Manyika akiwa katika viwanja vya Mliman City tayari kwa kutoa huduma
Afisa Habari wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Sheila Mfunami akifafanua jambo kwa mteja, Bw. Frank Mmbali katika maonyesho ya Brela yanayoendelea Viwanja vya Mlimani City. Brela imepiga kambi ya siku tano kuanzia leo January 26-30, 2022

Wananchi wakisubiri huduma. Brela imepiga kambi ya siku tano kuanzia leo January 26-30, 2022


 




Na Suleiman Magali

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imetoa  wito kwa wakazi wa Dar es salaam kutumia fursa ya maonyesho ya siku 5 yanayofanyika katika ukumbi Mliman City, kujitokeza kwa wingi ili kupata usaidizi wa changamoto wanazokumbana nazo kwenye kusajili biashara zao.

Wito huo umetolewa na afisa leseni na biashara wa Brela, Bi. Sada Kilabura jana, Januar 26, 2022 Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari viwanjani hapo.

 Alisema maafisa wa wakala wamejipanga vizuri kuwahudumia wananchi na kwamba hawatatumia muda mwingi kupata huduma.

“Kw majina naitwa Sada Kilabura, Afisa leseni kutoka Brela, tumeandaa maonyesho haya ili kutoa elimu kwa umma kuhusu huduma zinazotolewa na Brela, tunatoa huduma za kuandikisha majina ya biashara, Kampuni, alama ya biashara na huduma.

Pia tunatoa leseni za viwanda pamoja na kutoa leseni za biashara kwa daraja A, maonyesho haya ni fursa kwa wakazi wa Dar es Salaam kufika na kupatiwa huduma hasa kwenye changamoto zao wanazokumbana nazo.

Tupo hapa kwa siku 5, kuanza Januari 26 hadi 30, 2021, Nitowe wito kwa wafanya biashara wote, wadogo na wakubwa, waliosajiliwa na ambao bado hawajasajiliwa, wajitokeze Mlimani City.

“Inawezekana kabisa kuna baadhi ya wateja walisajiliwa kwa njia ya makaratasi, sasa hivi wanatakiwa kuhuisha taarifa zao kwa njia ya mtandao, hapa ndio sehemu sahihi ya kuja kupata usaidizi.

Aidha alisema kwa wale ambao bado hawajajiunga na huduma ya mmiliki mwenye manufaa (Beneficial owneship), tunawaomba wafike hapa kupata usaidizi.

Aidha kwa upande wao wananchi waliohudhuria maonyesho hayo wamesifu huduma inayotolewa na maofisa wa Brela, wakisisitiza kuwa wanawapokea vizuri na kutatua kero ambazo wanakumbana nazo katika kuhuisha taarifa zao.

“Huduma tulizopatiwa hapa Mliman City ni nzuri, zimejaa upendo, nawashauri wale wenye nia ya kuanzisha Kampuni/ au kusajili majina ya biashara yao wasisite kufika Mliman City kupata huduma,” alisema Marco

Aidha Marco Luena  ameongeza kusema kuwa aliwahi kupata shida kwenye kujaza taarifa zake katika mtandao lakini alipofika Mliman City maafisa wa Brela walimsaidia.

Naye Frank Mambali kutoka Ilala amesema ili kufanikiwa katika biashara ni lazima isajiliwe, changamoto kubwa aliyokuwa akiipata ni jinsi ya kuwafikia maafisa wa Brela, kwani mara nyingi wakifika ofisini kunakuwa na foleni za wateja, lakini kitendo chao cha kuamua kutoka ofisini na kuwafuata wateja waliko kinasaidia sana kuharakisha michakato ya usajili.

BRELA inatoa huduma mbalimbali zikiwemo usajili wa majina ya biashara, usajili wa alama za biashara na huduma, usajili wa makampuni, kutoa hataza kwa maana ya hati miliki kwa vumbuzi ambazo zinasaidia kutatua changamoto katika jamii”.

No comments