Zinazobamba

Brela yapata mwitikio mkubwa Mliman city, Wafanyabiashara ‘bubu’ wapewa rai

 



Afisa leseni na biashara wa Brela, Bi. Sada Kilabura akizungumza na mteja alifika Mliman City Kupata huduma.

Afisa leseni wa Brela, Bw. Robert Mashika akizungumza na wateja. Mashika amesema zoezi la usajili limeitikiwa vizuri na kwamba anaimani mpaka siku ya kufunga jioni watu wengi watakuwa wamefikiwa.
Afisa leseni Robert Mashika akizungumza na Kituo cha Redio Imaani iliyopo mjini Morogoro kwa kutumia njia ya simu, wasikilizaji wa kituo hicho walipata bahati ya kupata elimu juu ya huduma za Brela.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kupatiwa huduma Mliman City.

Na Suleiman Magali

Ikiwa leo ni sku ya pili toka kuanza kwa maonyesho ya siku tano ya utoaji huduma za Brela katika Parking za Mlimani City Jijini Dar es salaam, imeelezwa kuwa mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa ukilinganisha na siku za awali.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Afisa leseni wa Wakala wa usajili wa Biashara (Brela), Bw. Robert Mashika amesema zoezi la usajili limekwenda vizuri kwani Zaidi ya wananchi 200 wamefanikiwa kupata huduma ikiwamo usajili wa majina ya Kampuni pamoja na kusikilizwa

Mtaalam huyo wa masuala ya leseni amesema mbali na idadi hiyo ya wananchi waliofanya jitihada za kufika viwanja vya Mlman city na kusikilizwa lakini pia dalili zinaonyesha kutakuwa na ongezeko la watu hapo siku za usoni kabla ya kumaliza maonyesho yao siku ya jumapili.

Fullhabari ambayo ilifika viwanja vya Mliman City Mapema ilishuhudia Wananchi wakipatiwa huduma, huku wengine wakipatiwa vyeti papo kwa papo.

Huduma ambazo zimekuwa zikitolewa viwanjani hapo ni pamoja na usajili wa Nembo ya Biashara, hataza, hati vumbuzi na usaidizi wa kujaza taarifa katika mtandao.





Aidha amewataka wananchi wote hususani wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na viunga vyake kuchangamkia fursa hiyo ili kupata majibu ya maswali yao na ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili zikiwemo mifumo ya mtandao.


Wananchi wasifu ubunifu, watoa rai

Wakizungumza na vyombo vya habari mmoja wa wananchi aliyejitokeza uwanjani hapo Bw. Ramadhani Mmanga ametoa rai kwa wafanyabiashara wengine kuhakikisha wanasajili biashara zao ili wafanye kazi kisheria.

Naye Mohammed Mseja ambaye  alifanikiwa kusajili Biashara yake na kupatiwa cheti chake papo kwa hapo hakusita kuonyesha furaha yake hasa baada ya kupata cheti chake.

.

Pia Mseja ameungana na Mmanga kuwashauri wakazi wa Dar es Salaam kujitokeza katika viwanja vya mliman City ili kusajili biashara zao ili waweze kunufaika na mbambo mbalimbali

Ends,

 

No comments